Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la viwanja vya michezo. Viwanja vya michezo vingi katika halmashauri mbalimbali hali yake ni mbaya sana, ili kuboresha michezo ni lazima tuboreshe viwanja vyetu katika halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kukuza vipaji kuanzia shuleni ili tuwe na matokeo chanya ni lazima tuwekeze kwa watoto wadogo hasa kuandaliwe syllabus maalum zitakazowajenga wanafunzi wakiwa mashuleni ili kuwakuza kulingana na vipaji walivyonavyo ili kulisaidia Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vazi la Taifa. Kulingana na umuhimu wa jambo hili ni vyema suala la Vazi la Taifa lipewe kipaumbele kwani kutokuwa na Vazi la Taifa ni vigumu kumhukumu kwa kosa la mavazi, sio sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Suala la Kufungia Magazeti; jambo hili liangaliwe upya kwani magazeti yanasaidia kufikisha ujumbe kwa jamii. Naiomba Serikali ibadilishe utaratibu, badala ya kufungia gazeti apewe adhabu Mhariri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wasanii kufungiwa wakati nyimbo tayari zimepigwa kwenye redio na TV, jambo hili si sawa kwani huwezi kufuta wakati wimbo huo unakuwa umesambaa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, michezo irejeshwe mashuleni, UMISETA na UMITASHUMTA miaka iliyopita vyombo hivi vilichangia sana kukuza michezo na kuibua vipaji vingi kwa wanafunzi wetu shuleni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sera ya michezo ifanyiwe marekebisho ili kuleta ufanisi katika michezo nchini kwani tumekuwa tukifanya vibaya mara kwa mara katika Taifa letu.