Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada ya Serikali chini ya Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na wataalam wote ndani ya Wizara hii wanafanya majukumu yao kwa tija na ufanisi katika kurejesha heshima na sifa za Kitaifa kwa nchi yetu. Napenda kupata ufahamu kwa nini bajeti ya 2018/2019 imepungua kwa asilimia 15.4 kwa Sh.5,136,989,000/= kwa mwaka 2017/2018.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, bajeti ya mishahara ya mwaka 2018/2019imepungua kwa asilimia 11.7 kutoka Sh.17,276,616,000/= na kufikia Sh.15,253,265,000/= je, ni kutokana na punguzo la watumishi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini kilichosababisha bajeti ya matumizi mengineyo kuongezeka kwa asilimia 50.8 ya Sh.4,780,331,000/= kutoka lengo la 2017/2018. Wakati bajeti ya miradi ya maendeleo ni Sh.8,700,000,000/=, pungufu ya Sh.696,410,000/= ya bajeti ya matumizi mengineyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tunahitajika kuendeleza na kuimarisha maendeleo ya utamaduni na sanaa, maendeleo ya sanaa na maendeleo ya michezo na kutuwezesha kuibua vipaji vya aina zote na kuitangaza nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.