Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakushukuru. Sana nitatoa ushauri tu kwa sababu na mimi nimeshawahi kukaa huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza hakuna nchi yoyote duniani inaweza kuendelea kimichezo bila kuwa na makocha wake wazawa. Ni aibu kubwa kwa Taifa la Tanzania leo kuchukua makocha kutoka Burundi kuja kufundisha timu zetu za Premier League. Kocha Msaidizi wa Simba anatoka Burundi, Mbeya City - Burundi, Mbao FC – Burundi. Katika FIFA ranking Tanzania iko juu kuliko Burundi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nadhani ni wakati wa Serikali sasa kuwekeza ku-train makocha. Hata kwenye michezo ya Commowealth juzi, mabondia wetu walikuwa wanasimamiwa na makocha kutoka Kenya kwa sababu makocha wetu hawana sifa za kukaa kwenye ring. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni viwanja vya michezo. Ni kweli viwanja vyetu katika mikoa yetu vingi, hivi vya mpira wa miguu vinamilikiwa na Chama cha Mapinduzi, lakini havipo kwenye hadhi nzuri. Ushauri wangu ni kwamba ili utoe product nzuri ya wachezaji lazima uwe na viwanja vizuri. Niiombe Serikali, wala siyo dhambi, kila mkoa Majimaji, Mbeya, hebu ikiwezekana wakae na Jeshi, JKT wanaweza ku-maintain hivi viwanja na vikawa katika ubora mzuri zaidi, wao wakawa wanachukua kamisheni kama Chama cha Mapinduzi. Viwanja hivi vitakuwa na ubora sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda Misri, ukienda Port Said, ukienda Ismailia, viwanja vyote ni vizuri kwa sababu vinakuwa maintained na Jeshi. Badala ya JKT kushughulika na mikopo ya matrekta, huu ni wakati sasa wa ku-maintain viwanja hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu wa tatu. Leo tuna wachezaji wengi sana wa kigeni hapa Tanzania na tuna mokocha wengi wa kigeni hapa Tanzania. Kama kuna kosa ambalo mchezaji anayecheza kwenye nchi nyingine as an International Player or Profession anaweza kupata kosa kubwa sana kama atakwepa kodi. Lionel Messi alipata matatizo, Christiano Ronaldo alipata matatizo kwa sababu ya kukwepa kodi, Tanzania wachezaji wetu hawa wa kigeni hawalipi kodi na hata registration fee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchezaji anasajiliwa kwa milioni themanini lakini anachukua hiyo fedha anaondoka nayo kwenda nyumbani kwao, Serikali inakosa mapato. Niwaombe BMT hili jambo waliangalie. Kuna wachezaji wamesajiliwa hapa kutoka Zimbabwe, kutoka Uganda, kutoka Kenya, kutoka Ivory Coast, kutoka Benin na wengine hawana hata kiwango, lakini fedha anayolipwa kama registration fee haitozwi kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kwamba, leo hata ukimuuliza Mheshimiwa Waziri pale kwamba, hebu tuambie tu wachezaji wa kigeni kwenye registration fee walilipa kodi kiasi gani? Sidhani kama ana majawabu? Huu ndio ushauri wangu ambao nimependa niutoe leo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho, nchi zilizoendelea kimichezo duniani fainali za FA zinafanyika Makao Makuu ya nchi ile husika, lazima tuwe na huo utamaduni kuliko mwaka jana tumecheza Dodoma, mwaka huu Arusha, keshokutwa utasikia Chemba, kutoka Chemba utaenda kucheza wapi, Mafia, eeh! Au kwa Mheshimiwa Kakoso kule. Tuwe na msimamo kwamba fainali ya FA inachezwa kwenye Makao Makuu ya Nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.

Ahsante sana.