Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. PETER A. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nampa pole Mbunge mwenzangu Mheshimiwa Heche kwa kufiwa na mdogo wake ambaye ameuawa akiwa Kituo cha Polisi. Kauawa ndani ya mikono ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme, Wizara yetu ya Michezo pamoja na mambo yake yote inayofanya; na leo ameongea mwenzangu hapa, anasema viwanja ambavyo CCM ilivichukua kwa kuwa wameshindwa kuvifanyia kazi iwasaidie kuviendeleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala kwanza haliwezekani. Kama mmeshindwa kuviendeleza viwanja ambavyo mmepora kwa wananchi, tena mpaka sasa wananchi tuwape fedha za kuviendeleza, this is not fair. Kama vimewashinda, mvirudishe kwetu tuviendeleze kwenye Halmashauri zetu ili wananchi wetu waweze kufanya michezo na Taifa liendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano hata kule kwangu Ifakara, nina kiwanja kikubwa sana, CCM wamekipora. Kile kiwanja kimejengwa na wananchi kwa jasho la wananchi. Leo hii eti ni cha CCM. CCM hawana nyaraka yoyote, wame-forge nyaraka, haiwezekani. Kwa hiyo, naomba kwamba kama vimewashinda, mvirudishe kwetu tuvifanyie kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, Taifa lolote linatakiwa liwe na taswira ambayo inajenga heshima kwake. Taifa kama lina mambo ambayo hayaeleweki linakosa heshima kama ambavyo sisi kama hatueleweki tunakosa heshima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kwenye Taifa letu tumeweka kanuni mpya za mitandao. bloggers leo wanaambiwa wachangie Sh.100,000/= ili waweze kupeleka habari. Sisi kama Taifa kama tunashindwa kuwasaidia wananchi wetu wapate taarifa kama Taifa, watu wanajitegemea wenyewe, wanaweka mipango yao, tunakuja tunawakatisha tamaa, hatuwezi kuendelea. Juzi hapa Mheshimiwa Rais amesema hatuwezi kuwa na mitandao kama China. Kama tunaweza kuiga ya China hayo, tuige pia na kunyonga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, China kule kama mtu anafanya makosa ya rushwa mashtaka yao ni kifo tu. Hukumu ni kifo. Sasa kama hili la China ni zuri, pia wachukue na hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani wananchi wetu wanashindwa kupata taarifa za kimsingi, magazeti wanayafungia, tena wanayafungia kwa jambo hilo hilo ambalo linafanywa na mtu wa kawaida. Likifanywa kwa ajili ya kuisema Serikali jambo hilo hilo Mheshimiwa Waziri anasimama anachukua hatua; jambo hilo hilo likisemwa kwa ajili kumtukana Mwenyekiti ama Kiongozi wa Upinzani, Serikali wanakaa kimya. This is not fair. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kujenga Taifa ambalo watu wanakuwa treated kwa mujibu wa matakwa ya kiongozi aliyeko madarakani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Taifa letu linaongozwa kwa mujibu wa sheria; Taifa letu haliongozwi kwa mujibu wa maneno ama kwa mujibu wa kauli za kiongozi yeyote yule. Tuna sheria zetu, lazima tuzifanyie kazi. Haiwezekani tu mtu anasimama anasema kuanzia leo... (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)