Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa mchango wangu kidogo katika Wizara hii muhimu kwa maendeleo ya Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunamshukuru Mungu kwa mvua zinazoendelea katika nchi yetu pamoja na kuwa zimeleta madhara makubwa sana. Mfano, vifo kwa ndugu zetu na uharibifu mkubwa sana wa miundombinu ya barabara na madaraja. Ninapenda kujua Serikali ina mpango gani wa haraka kuhakikisha miundombinu hiyo niliyoitaja inatengenezwa ili kuondoa usumbufu mkubwa wanaoupata wananchi wetu kwa sasa uweze kuisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu nyumba za TBA Dodoma, mimi ni mmoja kati ya wapangaji wa nyumba hizo ila nyumba hizo kwa sasa ziko kwenye hali mbaya, zinavuja, matengenezo hayafanyiki kabisa, tunafanya wenyewe, kibaya zaidi hali iliyopo sasa hivi mazingira yanayozunguka nyumba zetu ni mabaya sana, majani yamekuwa marefu sana yanahatarisha usalama wa maisha yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni kutokuzolewa kwa takataka kwenye maeneo yetu na hii kunaweza kuibua magonjwa ya kuambukiza mfano kipindupindu. Tunaomba sana usafi na matengenezo hayo niliyoonesha hapo juu yafanyiwe kazi ili kulinda afya za wapangaji wa nyumba hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi ya kutoa mchango wangu huo, naamini niliyoyasema yatafanyiwa kazi kwa haraka hali ni mbaya, hasa nyumba zilizoko Area D Site Two, uchafu umezidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.