Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuunga mkono hoja. Nashukuru na kupongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa namna ilivyotekeleza Ilani ya Uchaguzi na utekelezaji wa maamuzi magumu na yenye tija ya Mheshimiwa Rais katika kuboresha sekta ya uchukuzi kwa vitendo. Niwapongeze pia Waziri mwenye dhamana na Naibu Mawaziri wake kwa kazi kubwa na yenye tija kwa Taifa wanayoifanya kwa ushirikiano mkubwa na watendaji wao. Hongereni sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu katika miradi ya barabara, barabara ya Nyakato – Buswelu – Mhonze kilometa 18, kwa miaka mitatu mfululizo inawekwa kwenye bajeti lakini hadi sasa ni kilometa 1.2 tu imekamilika. Niombe walau kilometa 17 zilizobaki ziingie zote katika bajeti ya 2018/ 2019 ili tuondoe adha hiyo ukizingatia barabara hiyo inapita Makao ya Wilaya. Aidha, mkandarasi JASCO aliyepewa zabuni hiyo hana uwezo, ikiwezekana aondolewe. Katika bajeti imetegewa kilometa moja tu. Ninachelea kusema Awamu ya Tano itakwisha bila kukamilika barabara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe ukamilishaji wa matengenezo ya kivuko cha Kayenze – Base ambacho kiliwekwa kwenye bajeti ya mwaka 2017/2018 na kinaonekana tena katika bajeti ya mwaka 2018/19. Naomba ukamilishaji wake ili kusaidia wananchi wa Kisiwa cha Base.

Mheshimiwa Naibu Spika, fedha za Mfuko wa Barabara; matengenezo ya Sabasaba - Busweru road, tayari Halmashauri inaendelea kulipa fidia kwa wananchi. Niombe utekelezaji wake ukamilike kama ulivyopangwa ili kurahisisha mawasiliano na Makao Makuu ya Wilaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa barabara za lami, mzunguko wa barabara za lami katika Manispaa ya Ilemela ni asilimia sita tu. Naomba ukamilishaji wa malengo yaliyowekwa ili hadhi ya Manispaa ilingane lingane na Manispaa zingine nchini.