Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. EMMANUEL J. PAPIAN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hata kama ni dakika kidogo. Nakushukuru sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza ninalotaka kuzungumzia, nimekuwa nashauri sana juu ya Benki ya Kilimo. Nimeomba mara nyingi sana kwamba hii Benki ya Kilimo ina mtaji mdogo, nimeomba zile pesa za TIB zihamie Benki ya Kilimo; nimeomba zile pesa za Mfuko zilizoko Exim zihamie Benki ya Kilimo ili benki yetu iwe na mtaji wakulima na wafugaji wetu waweze kukopa kwenye benki moja ili waende kwenye chombo kimoja, wapate huduma mahali pamoja, warejeshe malipo yao mahali pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba hii benki ihamie Dodoma. Kwa nini benki ikae Da es Salaam kwenye yale majengo maghorofa yanayolipa gharama kubwa! Majengo yapo Dodoma katikati ya nchi, anayetoka kusini aingie, anayetoka Kaskazini aje, anayetoka Magharibi aje lakini naomba hii Benki ihamie Dodoma. Hilo ni jambo la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili nililotaka kuzungumza ni hili suala la migogoro ya wakulima na wafugaji. Migogoro ya wakulima na wafugaji mara nyingi ukikuta mahali kuna mgogoro, wakulima na wafugaji wanapigana, mwanasiasa anafaidika na ule mgogoro. Watendaji wa Serikali wanafaidika na ule mgogoro!
Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali iangalie ni namna ipi tunaweza kufanya ili kuhakikisha kwamba mgogoro unapotokea mahali, unakabiliwa kwa wakati, wale Watendaji wa Serikali, Mwanasiasa anayeshiriki katika hilo, achukuliwe hatua haraka na Serikali ijulishwe na wananchi wajue ili kuweza kuhakikisha kwamba tunakabiliana na migogoro inayotokea baina ya wananchi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nizungumzie NARCO. Ukitaka kuitafuta Wizara ya Mifugo, lazima utaitafuta NARCO; ukitaka kuzungumzia mifugo nchini, lazima uitafute NARCO. Wabunge wengi wamezungumza habari ya mashamba yaliyoko huko Kalambo, Kagera, Arusha, Tanga; NARCO ndiyo yenye maeneo makubwa, lakini NARCO haipewi mtaji. Kwa nini haipewi mtaji? Nilishaomba nikasema, NARCO iombewe pesa za nje zenye riba nafuu ikopeshwe, mashamba yajazwe mifugo, tuajiri wataalam waingie pale, tuwasainishe mikataba, wakishindwa, ni Magereza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mashamba yako wazi, wafugaji pembeni wanayavamia, mwisho wa siku inaleta migogoro. Ndiyo maana inafika mahali watu wengine wanasema haya mashamba yachukuliwe, yanyang‟anywe. Haya mashamba yanakwenda wapi na ndiyo jicho la Wizara! Hakuna mahali pengine unaweza kuiona mifugo au kufanya researches? Watu wengi, sasa hivi wataalam wetu na vijana wengi wanaofanya Ph.D, Masters, kwenye fields wanakwenda kwenye hayo maeneo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba na kuishauri Serikali kwamba iombe pesa za nje kwa ajili ya NARCO, i-inject pesa za kutosha, iongeze wataalam tuweze kusimamia hayo maeneo na tuweze kufanya kazi kwa kuingiza mapato kwa maana nzima ya hiki Kitengo chetu cha Mifugo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikiwa kwenye Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa, mikoa ilipokuja juzi Dar es Salaam, nilikuwa nawaambia kila mkoa ujaribu kuainisha ni mazao gani yanaweza kustawi lakini ambayo ni commercial. Tusi-base kwenye mahindi, mwisho wa siku tukivuna, yanakuwa mengi, hayana soko. Mikoa ikiweza kuainisha yale mazao kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, yale mazao ya biashara; ufuta, alizeti na kadhalika yanaweza kusaidia mazao yakatoka nje tukaingiza foreign currency badala ya ku-depend on haya mazao ambayo asubuhi na jioni hatuna bei, bei imepatikana, haipo na internal collection bado haipo.
MHE. EMMANUEL J. PAPIAN: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kushukuru, naunga mkono hoja. Ahsanteni sana.