Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naunga mkono hoja. Nampongeza Waziri, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuikumbusha Serikali kwamba uwanja wa ndege Tanga unatakiwa kuboreshwa kama viwanja vingine kwa sababu uwanja huo utatumika sana baada ya bomba la mafuta toka Hoima hadi Tanga. Kwa hiyo, kutakuwa na wageni wengi watakaokuja Tanga kupitia usafiri wa ndege vikiwemo viwanda vingi vilivyopo na vinavyokusudiwa kujengwa pamoja na utalii uliopo Mkoani Tanga. Hivyo naiomba Serikali kuangalia uwanja huu kwa kutengea bajeti ya marorosho.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu barabara za lami Korogwe Mjini, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliahidi kilometa tano za lami ndani ya Mji huo. Niombe Serikali ahadi hii kama inawezekana ni kutoa kilometa 2.5 kila mwaka itakuwa imekamilika ahadi hiyo ndani ya miaka miwili tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, TARURA wanafanya kazi nzuri lakini bajeti waliyopewa ni ndogo. Ni kwa nini wasigawane nusu kwa nusu na TANROADS ili kuwawezesha TARURA kuwa na uwezo wa kutekeleza miradi ya barabara kwa uhakika. Vinginevyo ile shilingi 50 ya lita ya mafuta (disease/petrol) itolewe kwa TARURA ili kuwapa nguvu zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara za Mji wa Korogwe zinaharibika sana kwa mvua kutokana na Mji huu kuwa bondeni, ushauri wangu ni kwamba barabara zinazojengwa kwa kiwango cha changarawe zijengewe mitaro au mifereji ili kusaidia kupunguza uharibifu. Kwa msingi huo tunaomba kupewa fedha kwa ajili ya ujenzi wa mitaro/ mifereji.