Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara kutoka Geita (Nyankungu) kwenda Kahama, barabara hii ambayo inapita Nyang’hwale kwenda Kahama ni kiungo kikubwa kwa Mkoa wa Geita na Shinyanga, na hii sasa inatumika sana kwa usafirishaji wa bidhaa mbalimbali zinazotumika mgodini. Tunaomba ijengwe kwa kiwango cha lami kama ahadi ya Mheshimiwa Rais ilivyokuwa mwaka 2015. Hivi sasa barabara hii ni mbovu sana kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Uwanja wa Ndege Geita Mjini, Mheshimiwa Waziri kumekuwepo maneno mengi kuhusu ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Chato. Sisi wananchi wa Geita hatuoni tatizo la ujenzi wa uwanja wa Chato. Tatizo tulilonalo ni umbali wa huduma hiyo kutoka Geita Mjini kwenda Chato, ndio utakuwa uwanja wa watu wa Geita Mjini; maana yake mtu atatakwa kusafiri kilometa 184 kutoka Geita kwenda Chato au kusafiri kilometa 120 kutoka Geita kwenda Mwanza Mjini na kwa sababu hiyo tatizo na uhitaji wa Uwanja wa Ndege Geita Mjini lipo pale pale. Ushauri wangu ni kwamba uwanja wa CCM uliopo hivi sasa ukarabatiwe na kuwa na uwezo wa kutumika kwa shughuli zote abiria wa Geita na CCM na kinachoweza kufanyika ni kutofautisha jengo la abiria peke yake hakuna sababu ya kuanza ujenzi wa eneo jipya.

Kuhusu barabara za Mjini Geita, Mheshimiwa Waziri tulipewa ahadi ya kilometa 10, ahadi ya Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli wakati wa kampeni yake mwaka 2015. Kwa kuwa muda uliobaki, sasa ni miaka miwili tu naiomba Serikali kutimiza ahadi ya Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kwa kuwa hali ya barabara za Mji wa Geita ambao ni makao makuu ya Mkoa wa Geita ni mbaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ubovu wa vivuko vya Kigongo Busisi, Mheshimiwa Waziri vivuko hivi vimechoka sana na vimekuwa vikisababisha usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa kivuko, zipo nyakati feri inabaki moja tu magari na abiria wanakaa hapo zaidi ya masaa 10 kusubilia feri. Naiomba Serikali kuja na suluhisho lingine la mahali hapo.