Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nachukua fursa hii kuipongeza Serikali, Mheshimiwa Waziri, viongozi na watendaji wote katika jitihada zote katika kuhakikisha sekta zote za Wizara hii zinafanya kazi kwa maslahi ya kuwaletea wananchi maendeleo.

Mheshimiwa Naibu Spika, michango/ushauri kuhusu Shirika la Posta; Serikali iongeze fedha ili shirika liweze kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kuweza kukabiliana na ushindani na kuongeza kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi. Serikali ione umuhimu wa kununua meli ya abiria kwa usafiri wa baharini kati ya Dar es Salam na Zanzibar kwa madhumuni ya kuwasaidia wananchi wanyonge ili waweze kumudu gharama za usafiri kwani usafiri wa kampuni binafsi au mtu binafsi bei zake ni za juu sana kwa mwananchi mnyonge na abiria wanahitaji huduma hiyo wanazidi kuongeza siku hadi siku.

Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika letu la Simu (TTCL); nashauri zitafutwe fedha za ziada ili shirika liweze kupanua wigo zaidi wa kutoa huduma za kuwafikia wananchi katika maeneo yote ya nchi yetu Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, TBA ikague nyumba zake zote na kuzifanyia matengenezo zile ambazo zinahitaji matengenezo ili nyumba hizo zisiendelee kuharibika zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naunga mkono hoja, Hapa Kazi Tu, Mheshimiwa Waziri piga kazi.