Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia hoja hiyo hapo juu hasa nijikite katika masuala ya miundombinu ya barabara zote za Jimbo la Mtera zilizopo TARURA. Mwaka huu 2018 mvua zimeharibu sana barabara zote, naomba Mheshimiwa Waziri atusaidie kupata fungu la matengenezo ya uhakika wa barabara hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri atupatie majibu ya uhakika kuhusu ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka barabara kuu ya kwenda Iringa pale Mlowo barabarani mpaka Mvumi Mission Hospital kama ambavyo Mheshimiwa Waziri aliwaahidi wananchi wa Jimbo la Mtera mwaka 2015. Naomba kujua ni lini barabara hiyo itajengwa? Ahsante.