Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na uwanja wa ndege Songwe. Nimetembelea uwanja wa ndege wa Songwe na kuona jinsi ambavyo hauna taa za usiku kwa ajili ya kufanya ndege zitue vizuri na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uwanja wa Mwanza, nashauri kwamba Serikali iboreshe uwanja huo kwani unahitajika sana. Pia nishauri jengo la kuongozea ndege ambalo limesuasua kwa muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu barabara za mwendokasi, ni wazi wananchi walifurahia ujio wa mwendo kasi, lakini Serikali imeshindwa kusimamia vizuri ili kuondoa kero zake.

Mheshimiwa Naibu Spika, jamii iliamini kuwa mwendokasi itakuwa suluhisho, lakini kero zake ni kubwa, magari ni machache hivyo watu hukata tiketi na kukaa muda mrefu pia kujazana kama njiti za viberiti. Hali hii inaondoa dhana ya usafiri salama Dar es Salaam. Niishauri Serikali mwekezaji kuongeza magari.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nishauri Serikali kuangalia jinsi gani inaweza kwenda na mwendokasi wa ujenzi wa reli hiyo hiyo ya Kenya ambayo inatoka Mombasa na inakaribia Nairobi na wote tunawahi soko la mizigo ya Congo. Iwapo sisi tutatumia umeme kwenye reli yetu wakati Kenya wanatumia mafuta, je, gharama zitalingana za kuchukua mzigo huo Congo? Kama sivyo Serikali itaenda kupata hasara.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mlandizi Chalinze, nashauri kwamba barabara hii Serikali iamue kufanya matengenezo ya kudumu badala ya jinsi ilivyo sasa ambapo inatengenezwa na kuweka matuta muda mfupi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua Mlandizi ni bonde la mpunga hivyo ni bora kuinyanyua ili kuzuia ile hali ya sasa ambayo kila inapotengenezwa inatitia.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara hii iwe na vipaumbele kwani imebeba miradi mingi kwa wakati mmoja kiasi imepelekea kushindwa kutekeleza mipango yote.

Mheshimiwa Naibu Spika, bandari, niishauri Serikali kuwa kazi ya kuanzisha bandari kila kona wakati kuna Bandari ya Dar es Salaam ambayo ina miundombinu mingi iboreshwe ili kuweza kukidhi matarajio ya uendelezaji wa bandari yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzisha bandari nyingine Bagamoyo tukijua kabisa bandari nyingine na zenye tija mfano Mtwara kubaki ikifanya kazi chini ya kiwango kitu ambacho si sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali juu ya ufungaji flow meter bandarini kuokoa ufisadi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu viwanja vya ndege, nashauri viwanja vya Taifa letu kumilikishwa. Nimesema hivyo kwani mashirika ya mafuta yanayoendesha biashara ndani ya viwanja hivyo yanamilikiwa wakati viwanja vyenyewe havina hatimiliki.