Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na TARURA, kwa kuwa fedha zilizotengwa kwa ajili ya TARURA ni ndogo na barabara za vijijini na mitaa ni nyingi na zinahitaji matengenezo makubwa, naomba Serikali itafute vyanzo vingine vya mapato kwa ajili ya TARURA kwa ajili ya kuboresha barabara vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara za vijiji na mitaa katika Mkoa wa Njombe ni mbaya, hazipitiki. Naiomba Serikali kuhakikisha fedha hizo za TARURA zinatengeneze barabara hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, fedha zilizotengwa kwa ajili ya kutengeneza barabara za Itoni - Ludewa, Njombe – Makete na Kibena – Lupembe – Madeke ni ndogo. Naiomba Serikali iongeze fedha hizo lakini pia fedha hizo zitolewe kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, kiwanja cha ndege cha Mkoa wa Njombe ni kibovu. Kiwanja ni pori ambalo linasababisha vibaka na majambazi katika viwanja hivyo. Pia wafanyakazi wa viwanja vya ndege wanapokea rushwa kwa wananchi ili kuweza kukatisha kwenye viwanja hivyo ambapo bado uhalifu ni mkubwa. Naiomba Serikali itengeneze kiwanja hicho haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uvunaji maji, mwaka huu kuna mvua kubwa zinanyesha nchi nzima, lakini hakuna juhudi zozote za Serikali kuandaa mabwawa ya kutunza maji haya kwa ajili ya kutumia wakati wa kiangazi. Naiomba Serikali iweke mkakati wa makusudi wa kutengeneza mabwawa makubwa yatakayotumika kwa ajili ya kuhifadhi maji hayo ambayo yatatusaidia kwenye kilimo cha umwagiliaji.