Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa pongezi nyingi kwa Mheshimiwa Waziri Profesa Mbarawa na Naibu Mawaziri wake wote, Mheshimiwa Kwandikwa na Mheshimiwa Engineer Nditiye. Nampongeza sana Katibu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Nampongeza Engineer Mfugale na Mkurugenzi wa SUMATRA kwa msaada mkubwa wa Jimbo langu la Nyasa, pia wa Bandari na Mfuko wa Mawasiliano.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru sana kwa jitihada kubwa iliyofanyika ya kuwezesha kuanza ujenzi wa barabara ya Mbinga – Mbambabay kwa kiwango cha lami na mkandarasi yupo site.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kukubali ombi letu la dharura la ujenzi wa Daraja la Mitomoni katika barabara ya Nyoni Liparambe – Mkende. Tunashukuru sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, mto umekula watu wengi sana huu kutokana na watu kuzama kwa vivuko hafifu. Tutaomba ujenzi huo upewe kipaumbele na hata katika utoaji wa fedha uwe first charge, bora tuchelewe kidogo maeneo mengine japo nayo ni muhimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ujumla mahitaji ni mengi lakini kwa kuwa sungura ni mdogo itoshe kushukuru, bila kusahau mawasiliano katika Kijiji cha Kihurunga na Liparambe Ndondo na kuboresha maeneo ya Ng’ambo na Chiwande. Karibuni Nyasa!