Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia katika haya yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuzungumzia kuhusu uharibifu wa barabara katika Mkoa wa Katavi hususani katika Jimbo la Kavuu. Kwa kuwa barabara ya Tabora - Mpanda imeharibika sana na imefungwa kwa muda; je, Serikali haiwezi kuongeza mabehewa kwa njia ya reli kutoka Tabora - Mpanda ili kuweza kuwapunguzia adha wananchi wa Katavi kwani mabehewa ni machache? Kwa hiyo, ni vyema yaongezwe kwa madaraja yote, yaani kwa maana ya mabehewa ya daraja la kwanza, la pili na la tatu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha na ninaunga mkono hoja.