Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri TARURA kwa kushirikiana na Halmashauri zetu wanunuliwe mitambo ya utengenezaji na kukarabati barabara zetu za vumbi. Mambo haya yamefanywa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kahama na Ushetu kwa udhamini wa Benki ya CRDB. Kama Wizara haina pesa, basi Wakurugenzi waruhusiwe kukopa Benki kwa masharti ya kibiashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa data nilizonazo seti nzima ya vyombo hivi ikiwa ni pamoja na malori, bulldozer, kijiko haizidi shilingi bilioni moja. Kwa kufanya hivi tutapunguza gharama za TARURA kwani hata hivyo haina pesa. Kwa asilimia 30 hii, haitoshi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo kuanzia mwaka 2014/2015 ATCL ilipata hasara ya shilingi bilioni 943 na mwaka 2015/2016 ilipata hasara ya shilingi bilioni 109.2 na mwaka 2016/2017 ilipata hasara ya shilingi bilioni 113.7

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi majuzi tumepokea ndege nyingine ya tatu. Naomba kuishauri Serikali iongeze bajeti kwa ATCL kwani kila mwaka hasara yake inaongezeka kwa asilimia 4.4. Hii shilingi bilioni 3.9 haitatosha kulipia gharama ya hasara ya mwaka wa fedha 2018/2019.