Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nachangia hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, niongelee kuhusu TEMESA; yapo malalamiko ya wafanyakazi kwenye kivuko kwamba hawana mikataba ya ajira na hivyo kukosa fursa za kujiendeleza na hata hawawezi kukopa katika vyombo au taasisi za fedha kama wafanyakazi wengine walioajiriwa Serikalini. Naomba Serikali ifuatilie jambo hili ili wafanyakazi hawa ambao wengine wamefanya kazi kwa muda mrefu wapate haki wanazopaswa kupata kutokana na kazi wanayofanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, meli ya MV Victoria ni muhimu kwa usafiri kati ya Mkoa wa Kagera hasa Wilaya za Muleba, Bukoba, Misenyi, Karagwe na Kyerwa. Wananchi wote hawa wanategemea meli hasa kibiashara. Mkoa wa Kagera umegeuka dampo ya magari ya abiria yanayosafirisha abiria kutoka Bukoba – Mwanza kwa njia ya barabara. Biashara zote kutoka Mwanza kwenda Bukoba na Bukoba – Mwanza zinapita barabarani. Wananchi wanapata hasara kubwa. Malori yanapoharibika yakiwa yamebeba ndizi, huiva na kuharibika na hivyo kuwasababishia hasara.

Mheshimiwa Naibu Spika, matengenezo ya meli hii ya MV Victoria yatakamilika lini na kiwango gani cha matengenezo kimefikiwa? Wananchi wa Kagera ambao maisha yamekuwa duni kwa kupambana na ughali wa maisha kwa bidhaa kupanda bei kutokana na kusafirisha kwa njia ya barabara.