Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri Profesa Mbarawa, Naibu wake Mheshimiwa Kwandikwa na Mheshimiwa Nditiye kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2017/2018 tulipitisha shilingi bilioni 12 kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Kahama – Bulyanhulu – Geita kwa kiwango cha lami. Hata hivyo, hadi leo Aprili, 2018 taratibu za kupata mkandarasi hazijakamilika na kazi hazijaanza. Mwaka huu 2018/2019 Serikali imependekeza bajeti ya shilingi bilioni 18 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kufahamu lini hasa mkandarasi atapatikana na kazi kuanza? Shilingi bilioni 12 za mwaka 2017/2018, kiasi gani kimetolewa na kimefanya kazi gani? Lini hasa mradi huu utakamilika?

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.