Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Waziri kwa kazi zinazofanywa na Wizara hii katika sekta zote za ujenzi, uchukuzi na mawasiliano. Kazi nzuri zimefanyika katika sekta ya ujenzi, barabara nyingi zimejengwa kwa kiwango cha lami na kiwango cha changarawe pamoja na madaraja makubwa ya nchi hii. Sasa kuna maandalizi kati ya Kigongo - Busisi kwa kuwa daraja hili linachangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi wa nchi za Afrika Mashariki na kati za Kenya, Rwanda, Burundi, Uganda, DRC na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kukamilika kwa daraja la Kigongo - Busisi kutaleta mapinduzi katika sekta ya uchukuzi kwani kwa sasa usafiri wa vivuko vya MV Sengerema na MV Misungwi vinazidiwa na wingi wa magari ya mizigo na magari ya abiria na kwa hakika ujenzi wa daraja hili litaleta tija. Pamoja na mgawanyo wa mamlaka za Wakala wa Ujenzi wa Barabara wa TANROADS na TARURA, bado naiomba TANROADS waendelee na utaratibu wa kuunganisha Mkoa wa Tabora kupitia Wilaya ya Urambo, Kaliua, Mkoani Tabora na Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, Mkoani Shinyanga Wilaya ya Mbogwe hadi Mjini Geita, Makao Makuu ya Mkoa wa Geita.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza TANROADS Mkoa wa Geita chini ya uongozi wa Meneja, Haroun Senkunku na msaidizi wake Ndugu Maribe pamoja na watumishi wote wa TANROADS Mkoa wa Geita wanafanya kazi nzuri ya kupigiwa mfano. Ujenzi wa barabara zote zinazojengwa na kusimamiwa na TANROADS Mkoa wa Geita zina kiwango cha kuridhisha. Ninachoomba na kushauri ni TANROADS kukichukua kipande cha Iboya – Bwendamwizo – Nyikundu - Ivumwa hadi Migo Wilayani Geita inaendana na barabara ya lami inayotokea Mjini Kahama kwenda Geita Mjini ambako ni Makao Makuu ya Mkoa wa Geita.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Wizara ione umuhimu wa kuimalizia barabara hii kwa kuwa kupitia Kikao cha Bodi ya Ushauri cha Mkoa wa Geita tuliomba barabara kutoka mji wa Ushirombo hadi Mbogwe kwenda Geita Mkoani, kilichotokea kipande ni sehemu hii ya maombi yetu ilichukuliwa na kipande cha Iboya - Bwendamwizo - Nyitundu - Ivumwa hadi Wigo kuelekea Mkoani Geita kiliachwa. Hivyo, naiomba Wizara isikie kilio chetu ikipandisha hadhi kwenda TANROADS ili Wilaya ya Mbogwe ipate barabara ya kuunganishwa na Mji Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa kazi kubwa za ujenzi wa bandari, reli, viwanja vya ndege, madaraja makubwa na meli za vivuko katika maeneo mbalimbali nchini. Hongereni sana kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.