Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Abdallah Haji Ali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kiwani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ABDALLAH HAJI ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu muweza wa yote. Aidha, nakupongeza wewe binafsi kwa kuongoza Bunge vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tena kwa mara nyingine napenda kuzungumzia mwenendo mzima wa safari za ndege nchini hususan ndege ndogo ndogo. Namuomba Mheshimiwa Waziri ikimpendeza atoe maelezo kuhusu jambo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, takribani ndege ndogo ndogo za karibu mashirika yote yanayotoa huduma kwa safari za ndani zinaendeshwa na rubani mmoja. Nakusudia kwamba nyingi ya ndege hizi zinaendeshwa na rubani mmoja tu bila ya rubani wa akiba. Ndege hizi pamoja na udogo wake zimewekewa viti vya rubani wa akiba lakini cha kushangaza hakuna siku utakuta kuna rubani wa akiba katika kiti kile.

Mheshimiwa Naibu Spika, viti hivi huwa vinatumika kupewa abiria jambo ambalo sio sahihi. Rubani ni binadamu kama binadamu mwingine anaweza kupata matatizo wakati wowote na mahali popote na mifano imeshatokea. Hivi karibuni tulisikia kwenye vyombo vya habari nadhani ilikuwa Marekani bwana mmoja alikuwa akitokea kiwanja kimoja kwenda kingine kwa safari za kawaida yeye na mkewe tu. Katika safari yao walipokuwa angani yule bwana ulimpata ubinadamu kulekule angani akaumwa na kufariki kulekule angani. Kilichomsaidia yule mama kwa bahati na yeye alipitia mafunzo ya urubani na aliweza kuiongoza ndege na kutua salama na kutoa mwili/maiti kwenda kuzikwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu ni kwamba naishauri Serikali itilie maanani juu ya kuwepo marubani wa akiba katika ndege za mashirika yote yanayomiliki ndege ndogo ndogo zinazotoa huduma ndani ya nchi na wasiachiwe vile viti vya rubani wa akiba kuviuza kwa abiria. Sina uhakika juu ya sheria zetu za anga hapa Tanzania juu ya marubani wa akiba, namuomba Waziri atufahamishe tupate uelewa mpana pengine ninavyodhani ni kinyume.