Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kusema machache. Niseme kwamba niko kwenye Kamati ya Kilimo, kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri tunaendelea kukupa hongera kwa kazi yako nzuri na timu yako. Hata hivyo, nina machache ambayo ningependa tuweke record sawasawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hiki kitabu cha Mheshimiwa Waziri ni record, kina kumbukumbu, nimekisoma chote. Ukurasa wa 116 kinaainisha msaada wa chakula uliotolewa; ameainisha baadhi ya Wilaya. Kwa takwimu hizi, tafisiri yake ni kwamba, takriban asilimia 65 ya nchi yetu ina upungufu wa chakula. Kitu ambacho ningependa tuweke record sawasawa, humu ndani Mheshimiwa Waziri unasema kuna msaada wa chakula mmepeleka kwa Wakimbizi. Sasa nataka tuweke record sawasawa, siku hizi NFRA ndiyo inalisha wakimbizi wetu au ni suala la UNHCR? Naomba tuweke record vizuri kwenye vitabu vyetu hivi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia bullet inayofuata umesema tumetoa msaada wa chakula Southern Sudan. Sasa tumerudi kwenye enzi za Mzee Nyerere za ukombozi wa Bara la Afrika? Kwamba sisi tunaanza kuwalisha watu wa Southern Sudan?
Mheshimiwa Naibu Spika, nilidhani kule Southern Sudan tunakwenda kuuza nafaka zetu, kwasababu kuna fedha za UNHCR! Nilihisi vilevile kwenye makambi ya wakimbizi NFRA inakwenda kuuza chakula kule ili tupate fedha, tena fedha za kigeni kwa sababu haya Mashirika ya Kimataifa yana fedha za kigeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tuweke record sawasawa, huo msaada unaosema unapeleka Southern Sudan ni msaada wa namna gani? Hao wakimbizi to my knowledge ni kwamba hawahitaji NFRA, wao wanalishwa kupitia fedha za UNHCR. Pengine Mheshimiwa Waziri kwa taarifa yako tu, sisi kwenye RCC tumeshakubaliana kwamba RC atakuja kwako kuomba kibali ili Mashirika ya Wakimbizi yanunue chakula katika Mkoa wa Kigoma ambacho kinazalishwa na wananchi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hilo tumeshakubaliana kwenye RCC na nasikia eti mpaka waje waombe kibali kwa Waziri. Mahindi ya kwetu, kuyauza NHCR hatuwezi mpaka tuje tuombe kibali kwenye Wizara. Nadhani hayo ni baadhi ya mambo ambayo yanahitaji kurekebishwa katika mfumo wa huu utawala wa nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ambalo ningependa niliseme, Mheshimiwa Waziri tumeshazungumza suala la uzalishaji wa mbegu na suala la Bugaga. Nimekupa options mbili; hili shamba la Bugaga maarufu shamba la Wajapani; shamba la mbegu tulilitoa kwa ASA. Huu ni mwaka wa nane limeachwa kuwa shamba pori. Sisi tumewapa option tu, kama hili shamba hamlihitaji turudishieni Halmashauri. Turudishieni shamba letu! Haiwezekani! Uhaba wa kuzalisha mbegu ni mkubwa, lakini huu ni mwaka wa nane, shamba limekaa, lina miundombinu ya umwagiliaji lakini halitumiki! Kama wenzetu wa ASA wameshindwa Mheshimiwa Waziri na Wizara yako imeshindwa kulitumia, tunaomba shamba letu mturudishie. Wala hatuna ugomvi na hilo, tutalitumia wenyewe na tuna uwezo wa kulitumia.
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine kwa kweli ni kwamba na Waheshimiwa Wabunge wote mtuunge mkono, tumuunge mkono Waziri tuhakikishe fedha za pembejeo zinaongezeka. Hatuwezi kuzungumzia uchumi wa viwanda wakati hatujatafsiri kibajeti kusaidia Sekta ya Kilimo, haiwezekani! Naomba Waheshimiwa Wabunge wote tushikamane wakati utakapofika tuhakikishe sekta hii inaongezewa fedha; fedha za mbolea, fedha za madawa na kadhalika na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo ningependa niliseme ni mbolea hii ya Mijingu. Mheshimiwa Waziri kuna maeneo mengi, mbolea hii ya Mijingu ambayo inazalishwa katika nchi yetu, wananchi hawaelewi vizuri, wanailalamikia! Kwa nini Wizara msije clearly na wewe Mheshimiwa Waziri na watalaam wako mkaeleza exactly utajiri wa mbolea hii ili wananchi waelewe? Kwa sababu mbolea hii inazalishwa nchini, tungekuwa na fursa ya kuitumia zaidi. Ni muhimu kabisa wananchi hawa waelewe contents za mbolea hii na umuhimu wa mbolea hii. Maeneo mengine mbolea hii watu wanaikataa, lakini Serikali imekaa kimya haisemi jambo lolote. Tokeni nje muisemee mbolea hii kwa sababu inazalishwa hapa nchini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, ni kumkumbusha tu Mheshimiwa Waziri na Watalaam wake wananisikia, kuna mtu mmoja amezunguza jambo hili; katika nchi yetu mikoa mitatu inayopata mvua za uhakiki inajulikana na ni Mikoa mitatu tu!
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa miaka 40 iliyopita mikoa yenye mvua za uhakika, udongo wa rutuba ni mikoa mitatu tu. Mkoa wa kwanza ni Kagera, hakuna uwekezaji wa maana umefanyika wa kilimo kule; Mkoa wa pili ni Kigoma, hakuna uwekezaji wa maana wa kilimo umefanyika kule; Mkoa wa tatu ni Katavi. Sasa mnahangaika, mnawekeza maeneo ambayo hayana mvua, hayana udongo wenye rutuba, ni kitu gani mnafanya Mheshimiwa Waziri? Mkae kama Serikali, hii Mikoa ambayo tuna comperative advantage, tuweze kuwekeza kwa nguvu zetu zote katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, pale Kasulu tuna Chuo cha Kilimo. Kile Chuo kilikuwa cha World Bank baadaye World Bank wakakiacha, sasa kimerudi. Tunaomba kupitia kwako Mheshimiwa Waziri na wananchi wa Kasulu wamenituma jambo hili, tunakiomba kiwe ni sehemu ya mlingano, sehemu ambayo…
MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii lakini Mheshimiwa Mwigulu nadhani tumeelewana vizuri.