Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kumshukuru Waziri, Naibu Mawaziri na watendaji wote kwa juhudi wanayoifanya katika kuitendea mema nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nijikite katika ujenzi wa barabara ya Tanga – Pangani - Saadani - Bagamoyo. Najua katika bajeti hii ya 2018/2019 barabara hii imo kwenye mipango ya kujengwa kwa kiwango cha lami. Naiomba Serikali ihakikishe barabara hii inajengwa kama ilivyopangwa katika bajeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ambayo inapitia Pangani - Saadani -Bagamoyo ina umuhimu sana. Kuna mbuga ya wanyama ya Saadani ambapo simba na tembo wanacheza pamoja katika ufukwe wa bahari wa maeneo ya Saadani yaliyopo karibu na Pangani. Barabara hii itasaidia kuleta watalii na kuweza kuliingizia Taifa fedha. Mbuga hii ni nzuri kwa hiyo ujenzi wa barabara utasaidia kukuza pato la Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuipongeza Serikali kwa kununua ndege ambazo ni hatua kubwa ya maendeleo. Katika Kata ya Bweni, Wilaya ya Pangani kuna hoteli inaitwa Mashadu. Hoteli hii ina kiwanja kizuri cha ndege ambapo ndege ndogo hutua kushusha na kupandisha abiria. Naiomba Serikali ifanye utafiti ili kama kuna uwezekano ndege ndogo za kwetu zitue katika kiwanja hicho kilichopo Mashadu, Wilaya ya Pangani.