Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa sababu muda wangu ni mdogo, naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri. Nawapongeza Serikali lakini tupongeze na jitihada za Mheshimiwa Rais kutaka ku- excel uchumi katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna ndege nzuri, jana nilikuwa nasikia mtu anasema ndege hizi hazifai. Ndege hizi zina store equipment system ambazo zina-show take off na landing, zinafaa kwenye viwanja vyetu vidogo ambavyo haviwezi kubeba ndege ambazo zinachukua runway ndefu sana. Kwa hiyo, tupongeze jitihada hizi za ndege hizi kuweza kutumika katika viwanja vingi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ndege hizi hazitumiki sawasawa kwa sababu viwanja vyetu havina ubora wa kupokea ndege husika. Hata viwanja vingine, kuna kipindi viwanja vyetu vinashindwa kuchukua ndege au ndege kutua kutokana na hali mbaya ya hewa, simply kwa sababu hatuna transponder instrument landing system ambazo katika mazingira ya hali yoyote ya hewa ndege hizi zinaweza kutua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tuweze ku-capitalize matumizi ya ndege hizi, kitaalam ndege huwa haipumziki, kinachopumzika ni rubani na crew ambao wako kwenye ndege. Kwa hiyo, tungekuwa na viwanja ambavyo vina taa, instrument landing system, precision approach path indicators na vertical approach slope indicators, itasaidia ndege hizi kuwa capitalized na kutumika kwa kipindi chote 24/7. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri alizingatie hili aboreshe viwanja ndege ziweze kuruka kwa usalama wa abiria, vifaa vyenyewe na viwanja vya ndege vyenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la reli hii ya SGR, ni hatua kubwa sana ambayo tumepiga na naipongeza Serikali. Reli hii kama haina mizigo itakuwa haiwezi kufanya kazi vizuri, haitaweza kulipa deni kwa muda unaotakiwa. Solution ya reli hii ni mizigo na bandari ya Dar es Salaam iko congested.

Mheshimiwa Mwenyekiti, licha ya kuwa kuna utaratibu wa mazungumzo lakini yasiwe taratibu. Mpaka leo ujenzi wa bandari ya Bagamoyo bado hakieleweki, bila bandari hii reli yetu itakosa mizigo na tutashindwa kurudisha pesa hizi mapema, tusiogope kukopa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba Serikali ijaribu na wataalam ambao wapo na wazuri wakae na mwekezaji wakubaliane twenty equivalent units za makontena yatakayoingia kwenye bandari ni mangapi, waweze kujua wharfage ya mwekezaji ni ngapi na duty ya Serikali ni ngapi. Tukienda hivi tutafanikiwa kujenga reli na bandari kubwa ya kisasa ya kuweza kubeba mizigo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu imekumbwa na mafuriko, mafuriko hayana nguvu mbele ya utaalam na engineering ya binadamu. Katika Bonde la Msimbazi ambalo linaanza kutoka Segerea linakwenda Surrender Bridge. Jambo ni dogo sana, Serikali wametuambia katika mpango wa DMDP wana mpango wa kuboresha mto huu, lakini wanakopa hizi pesa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wako watu ambao wamejitokeza ambao watalipa fidia na kutengeneza miundombinu ya mfereji huu, kwa nini hawa watu wasipewe kazi hii? Kwa nini Serikali mkope halafu katika kukopa kwenu hakuna component ya fidia?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama wananchi hawa hawatalipwa fidia sisi hatutakubali. Tunataka wananchi wetu walipwe fidia kwa sababu they have been there for the last sixty years. Kama kuna mtu kajitokeza ni bora afanye yeye na Serikali mkope kwa kufanya mambo mengine ili wananchi hawa waende katika sehemu bora zaidi na kuendeleza maisha yao. Hawa ndiyo watu walionipigia kura mimi lazima niwatete. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Dodoma - Dar es Salaam imeshakwisha, iko congested na ni ndogo. Namwomba Waziri, tayari wako watu wamejitokeza wa Kuwait Fund kui-finance barabara hii, wazungumze nao ili waweze kujenga barabara hii kwa njia sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maneno hayo, nikushukuru sana na naunga mkono hoja kwa kazi nzuri anayofanya Mheshimiwa Waziri na Serikali kwa ujumla.