Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza kabisa, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu; pili, naishukuru familia yangu na tatu, namshukuru Kiongozi wangu wa Kambi ya Upinzani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naenda kwenye upande wa uvuvi. Tanzania imekuwa ikiongoza Afrika Mashariki katika uvuvi wa ndani ya nchi na uvuvi wa maji baridi ambao ni kama mito pamoja na maziwa. Pia katika Maziwa Makuu, imekuwa ikiongeza pato la Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na uvunaji mkubwa wa samaki hali ambayo inahatarisha uvunaji endelevu wa samaki. Kwa mfano, sasa hivi samaki kama sato, sangara, wamekuwa ni adimu sana katika Ziwa Victoria na bei yake pia imekuwa iko juu. Kwa mfano, ukichukulia kuanzia miaka mitatu iliyopita, samaki aina ya sangara ulikuwa ukimnunua sh. 5,000/= samaki wa kilo tano au kilo saba, lakini sasa hivi samaki huyo hakamatiki kutokana na uvuvi holela. Je, ni mkakati gani ambao Serikali imeuandaa kwa mwaka wa fedha ili kukabiliana na changamoto hii? Kuchoma nyavu kumekuwa na ugumu mkubwa wa kupata fursa za mikopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naenda kwenye kilimo. Tanzania tumebarikiwa sana kuwa na ardhi ya kutosha na yenye rutuba. Mimi ninatokea Mkoa wa Mara; Mkoa wa Mara tulikuwa tunalima sana zao la pamba na pia tulikuwa na Kiwanda cha Mutex ambacho kilikuwa kinafanya kazi kubwa sana, kilikuwa kinasaidia sana vijana pamoja na wanawake kupata ajira. Pia kiwanda hicho kimekuwa kikiinua sana pato la Taifa. Leo hii kutokana na kutokuwepo na ulimaji wa pamba, imekuwa ni shida kubwa sana na kiwanda hicho kimefungwa na kimekuwa kikisuasua. Je, Serikali iko tayari kuinua zao la pamba ili kiwanda hicho kifunguliwe? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine, nitaongelea hapo hapo kwenye suala la kilimo. Mkoa wa Mara umepakana na nchi ya Kenya. Nchi ya Kenya imejikita sana kwenye zao la maua. Je, kwa nini Serikali yetu pia isijikite kwenye zao la Maua? Ukiangalia kwa mfano, Mkoa wa Mara umepakana sana na Wilaya ya Tarime ambapo iko karibu sana na nchi ya Kenya na hali ya hewa inafanana na nchi ya Kenya; kwa nini na sisi Tanzania tusijikite kwenye kilimo cha maua? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye upande wa mifugo. Mkoa wa Mara tuna ng‟ombe wengi wa kutosha, lakini wafugaji hawa wanatumia miundombinu ambayo si endelevu. Lazima Serikali ianze kuandaa mpango wa muda mrefu kwa ufugaji wa kisasa kwa sababu tutakapofuga kisasa itatusaidia sana. Pia Serikali iandae majosho na machinjio yawe ya kisasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa mwenzangu wa Mkoa wa Mwanza, amesema kwamba wao Wasukuma ni wanywaji wa maziwa na sisi wananchi wa Mkoa wa Mara ni wanywaji wakubwa sana wa maziwa na pia walaji wazuri sana wa nyama ya ng‟ombe. Kwa nini Serikali isiweke kipaumbele kuhakikisha kwamba hawa ngombe wanakuwa kwenye malisho mazuri kwa sababu maeneo mengi ya malisho hayapo. Maana mtu ukiwa na ng‟ombe zaidi ya 100 ni shida, utaenda kuwalishia wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunaomba Serikali iweke kipaumbele kwenye suala la mifugo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.