Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Kwanza nimpongeze Waziri, Naibu Mawaziri pamoja na watendaji wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayofanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na ujenzi wa barabara ya Mbande – Kongwa – Mpwapwa. Nashukuru kwamba Mbande - Kongwa imeshaanza kujengwa, wasiwasi wangu tukisubiri barabara hii ikamilike kuanzia Mbande - Kongwa junction ndiyo waanze kujenga barabara ya Mpwapwa kwa kweli itachukua miaka 30. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kwamba barabara hii ianzie kujengwa Mpwapwa kuja huku Kongwa, nadhani hii itakuwa rahisi zaidi. Mwaka jana nilisema sana, nadhani Wizara hii ni sikivu, wamenisikia, mwaka huu watanisaidia. Wananchi wa Mpwapwa wameikosea nini Serikali ya CCM? Tangu nimeingia Bungeni mwaka 1990 kila hoja naiunga mkono, sijapinga hoja yoyote. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais Mstaafu Mheshimiwa Mwinyi aliniahidi haikujengwa, Rais Mstaafu Mheshimiwa Mkapa aliniahidi haikujengwa, Rais Mstaafu Mheshimiwa Kikwete aliniahidi haikujengwa na Rais Magufuli ameniahidi. Kwa hiyo, nina hakika kabisa Profesa Mbarawa, Waziri wa Ujenzi mwaka huu asikilize kilio za wananchi wa Mpwapwa. Namwomba sana kwa unyenyekevu kabisa wanisikilize. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili nimeona hapa Mheshimiwa Waziri starting construction Gulwe brigde. Daraja la Gulwe linajengwa sasa sijui linajengwa daraja lipi lingine? Daraja ambalo limebomoka kwa kuchukuliwa na mafuriko ni daraja la Godegode. Sasa hivi wananchi wanapata shida sana, wanavushwa kwa Sh.2000 kama ni pikipiki Sh.5000. Kwa hiyo, namwomba sana Mheshimiwa Waziri, hii ni dharura wajenge daraja hilo ambalo ni kiungo kati ya Jimbo la Kibakwe na Jimbo la Mpwapwa. Kwa hiyo, na,womba sana Mheshimiwa Waziri ashughulikie daraja hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliomba barabara ya kutoka Gulwe – Berege – Chitemo - Mima mpaka Seruka ichukuliwe na Serikali. Kwa sababu wakati huo ilikuwa chini ya halmashauri wakasema hapana kwa kuwa tumeanzisha chombo TARURA, itajenga ile barabara. Ombi langu ni

kwamba TARURA wasigawane fedha na TANROAD, TARURA itengewe fedha zake za kutosha hizi za TANROAD ziachwe ili TANROAD ijenge barabara ya lami ya Mpwapwa – Mbande - Kongwa na barabara zingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono kwa asilimia mia hoja ya Mheshimiwa Waziri. Ahsante sana.