Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi niweze kuchangia kwenye hotuba hii nzuri ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Kipekee kabisa kwanza nimpongeze Waziri na timu yake ya Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wote kwenye sekta hizi, wanafanya kazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, niipongeze Serikali kwa miradi mikubwa ambayo inatekeleza, hii ya standard gauge, mambo ya ndege, upanuzi wa viwanda, viwanja vya ndege na kuboresha mawasiliano kwa ujumla mnafanyakazi nzuri. Kwa kuwa dakika tano ni chache basi naomba tu niipongeze Serikali kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza, mimi ninatokea Buhigwe, mawasiliano kwenye vijiji vyangu viwili yanahitajika. Tumeshaleta maombi kwa Naibu Waziri na ndani ya ofisi ya mawasiliano, Kijiji cha Katundu na Kijiji cha Kajana mawasiliano ni hafifu na kule wamenituma muweze kupeleka mnara ili waweze kwenda vizuri.

La pili, niipongeze Wizara kwa kuipandisha hadhi barabara zangu miaka iliyopita, ya Buhigwe, Muyama, Mgera na Katundu, mmeanza kuitengeneza vizuri. Nimpongeze kwa dhati kabisa Meneja wa TANROADS wa Mkoa wa Kigoma anafanyakazi nzuri sana. Miongoni mwa mameneja ambao wanatakiwa uwapandishe na uwape mshahara mkubwa ni meneja wa TANROADS Mkoa wa Kigoma, anafanyakazi nzuri sana, ni debe kwa sababu anafanyakazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe meneja wa TANROADS pale kwenye mto Mlangilizi pale kutokea Kijiji cha Migongo kwenda Mgera, tuna mto mkubwa ambao wameanza kuweka maandalizi ya kujenga lile daraja. Kwa hiyo naomba waweze kulimalizia kwasbabu bado ni kero kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna daraja lingine kwenye barabara hiyo, Mlela yeye anajua, ukitokea Buhigwe kwenda Muyama kuna daraja bovu sana pale tunalo; kwa sababu ile barabara imepanda hadhi; tungependa aweze kuimalizia. Vile vile barabara ile ya Mnanila - Mwayaya - Mbanga mpaka Janda ambayo ni ya TANROADS nayo tungeomba kwa safari hii iwekewe fedha ili iweze kutengenezwa kwa kiwango cha TANROADS kwa sababu Wilaya wana uwezo mdogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sijaona ahadi ya kilometa tano za lami kwenye kitabu chako, kwa sababu Mheshimiwa Rais alishaahidi kwamba atazitengeneza, sasa sioni kama iko kwako na kama kwenye kitabu chako hatuoona kilomita tano zinatengenezwa kwa namna gani, tungependa utupe ufafanuzi utakapokuwa una-wind up. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine ni ushauri. Shirika letu la TRC linafanya kazi nzuri na limeanza kwenda vizuri. Tunachokiomba wanapoahirisha watoe taarifa kwa wasafiri kwa sababu wanasumbuka sana, hawajui reporting yao na hamja-improve vizuri. Hata mnapofika Dodoma hamwendi Dar es Salaam basi muwataarifu, wanakaa waka- hang, wanatupigia simu, muwe mnawataarifu vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho; ningeomba muweze kumalizia jengo la abiria kwenye uwanja wa ndege wa Kigoma, kwa sababu uwanja umeshakuwa mzuri basi muweze kumalizia jengo vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina mengine, nawashukuru, endeleeni.