Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ni nzuri, nina issues za kuzungumza.

Kwanza napenda nipongeze sana miradi ya kimikakati ambayo inafanywa na Wizara hii; kwa mfano barabara, ujenzi wa reli, vivuko pamoja na ndege, ni miradi ya kimkakati na ni ya kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu dakika ni chache naomba niingie moja kwa moja kwenye hoja zifuatazo; kwanza tunahitaji kuwa na viwanja vya ndege ambavyo vya kimkakati vilevile. Uwanja wa Ndege wa Mwanza naomba sana Mheshimiwa Waziri utakapokuwa unajibu hapo utuambie lini jengo la abilia linajengwa Mwanza. Imekuwa ni hadithi ya muda mrefu, lakini bado uwanja wa Mwanza ni uwanja wa mkakati hata kiuchumi. Nakuomba sana tupate majibu kwa sababu hatuwezi tukawa tunaenda tunarudi, tufike mahali tuwe na uamuzi ambao ni sahihi. Kama ni fedha tenga fedha za ndani zianze kujenga Uwanja wa Ndege wa Mwanza. Vivyo hivyo uwekaji wa taa za kurukia ndege kwa Uwanja wa Songwe wa Mbeya nao ukamilike. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba vilevile kuhusiana na suala la barabara ya Nyanguge - Busega - Mara Border;ukitoka Mwanza mpaka Nyanguge barabara ni nzuri, ukifika border pale ya Mara na Simiyu kwenda mpaka Musoma barabara ni mzuri, kipande cha Nyanguge mpaka Mara Border ni kibovu sana na kila mwaka ukarabati unafanyiake fedha nyingi inatumika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachopenda kujua ni kwamba ni lini sasa barabara hii itarekebishwa kwa kiwango ambacho haitakuwa na usumbufu? Kwamba kila mwaka unaona wakandarasi wako barabarani? Inasababisha ajali na ni kipande ambacho ni muhimu sana; kwa hiyo ningepenga sana kujua hilo, pamoja na daraja la pale Simiyu, ukiwa pale Magu lile la chuma, ni barabara ya miaka nenda rudi mpaka leo hii ni single lane, yaani huwezi ukapishana pale na bado ni chakavu naomba lilekebishwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja suala la barabara ya Nyashimo - Ngasamo mpaka Dutwa kwa Mheshimiwa Mwenyekiti Chenge. Barabara hii Mheshimiwa Rais alihaidi kwamba ijengwe kwa kiwango cha lami, mpaka leo sijaona mkakati wowote wa kujenga kiwango cha lami. Nataka kujua Mheshimiwa Waziri atakapokuja ku-wind up ni lini barabara hii ya Nyashimo-Ngasamo-Dutwa itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Ni ahadi ya Mheshimiwa Rais, aliwaahidi wananchi wa Wilaya ya Busega na Wilaya ya Bariadi, tena wakamshangilia sana na kura zikawa nyingi sana. Naomba hili suala tusimwagushe Mheshimiwa Rais. Kauli ya Mheshimiwa Rais ni maelekezo tosha kabisa. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri utakapokuja hapa nataka kujua ni lini ujenzi wa barabara hii utaanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni suala la TTCL. Tunazungumza kuhusu kuboresha mashirika yetu, lakini taasisi za Serikali hazitaki kujiunga na mfumo wa kanzidata wa TTCL; Mheshimiwa Waziri umesema ni makampuni 52 tu, kwa nini ni makampuni 52 peke yake? Naomba kampuni zote na taasisi ya Serikali zitimize maelekezo ya Serikali na walipe madeni. Hizi taasisi au mashirika yasipolipa madeni ya Serikai inakuwa tunakwamisha shughuli za uendelezaji wa mashirika haya. Kwa hiyo, nilikuwa naomba sana mashirika haya ya weze kulipa pesa zake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia la mwisho kabisa nakupongeza wewe, lakini naomba hivi barabara ya Nyasimo - Ngasamo - Dutwa nipate majibu, ahsante sana.