Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu hongera kwa kazi nzuri unayoifanya wewe na Naibu wako na watendaji wako. Ni kazi iliyotukuka hadi mmewezesha Namtumbo tutarajie kuwa na huduma za upasuaji kupitia Kituo cha Afya cha Namkumbo kinachotarajiwa kukamilika kujengwa tarehe 31 Mei, 2018. Ahsante ninyi ndio mlitafuta fedha za ujenzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Namtumbo ni Wilaya kubwa nawaomba mtutafutie fedha zaidi kwa ajili ya kuendeleza nguvu za wananchi kupitia Halmashauri yao ya Namtumbo kukamilisha ujenzi wa vituo vya afya vingine viwili vya Lusewa na Mtakanini.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Lusewa kiliahidiwa kukamilishwa na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne pamoja na Makamu wa Rais wa Awamu ya Tano. Ni vyema ahadi hiyo ikatekelezwa ili wananchi wa Lusewa na Tarafa nzima ya Sasawala waache kuwabeba akina mama wajawazito wanaoshindwa kuzalishwa na waganga wa kienyeji kupakiwa kwenye baiskeli ndani ya matenga au machakacha kupelekwa Kiuma (Tunduru); Mbesa (Tunduru) au Songea umbali wa kilometa 72, 95 na 150; Mtawalia na ni wazi huwa hawafikishwi katika maeneo hayo yenye huduma ya upasuaji na huishia kugeuza safari, mama akibadilishwa jina kwa kuanzia na marehemu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kituo cha Mtakanini kiliombwa na Marehemu Mheshimiwa Rashid Mfaume Kawawa kwa Rais wa Awamu ya Tatu na Rais huyo Mheshimiwa Benjamin William Mkapa kukubali ombi hilo mbele ya familia na wanakijiji wote wa Mtakanini na ikakubaliwa kuwa ndio kiwe Kituo cha Afya cha Kata ya Msindo. Aidha, kituo hicho kitahudumia kata tatu, Kata za Msindo, Hanga na Namabengo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.