Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuishauri Wizara itathmini miradi yote iliyokuwa imefadhiliwa na Benki ya Dunia kuboresha baadhi ya zahanati kwa kujenga wodi za wazazi na theater ili kuboresha afya ya mama na mtoto.

Moja ya zahanati hizo ni Zahanati ya Itumba katika Jimbo la Igunga ambayo ilipewa mradi wa kujenga na kuboresha theater na wodi. Mradi huo ulimalizika bila kukamilishwa kwa majengo (miundombinu) hayo kwa miaka mitatu sasa. Naomba Serikali ikamilishe mradi huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, naiomba Serikali pia ikiboreshe Kituo cha Afya cha Igurubi ambacho uhudumia kata sita za Tarafa ya Igurubi za Kiningu, Igurubi, Kininginila, Mwameshimba, Itunduru na Isakamaliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.