Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Rukia Ahmed Kassim

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. RUKIA KASSIM AHMED: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa pongezi kwa Mheshimiwa Waziri wa Afya kwa juhudi zake za kupeleka Madaktari Bingwa katika mikoa ya pembezoni kwa huduma za kibingwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wengi walikuwa wakishinda kufuatilia huduma hizi Muhimbili jambo ambalo limeleta faraja kubwa kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na ongezeko kubwa la maradhi ya kisukari mpaka kwa watoto wadogo jambo ambalo limeleta hofu sana kwa wananchi wetu. Hivyo naishauri Serikali ifanye utafiti tuweze kujua sababu au chanzo cha maradhi hayo. Inawezekana pengine kuna vitu ambavyo vinasababisha ongezeko la kasi lililojitokeza la maradhi haya ya kisukari.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikia Mheshimiwa Waziri wa Afya akisema katika hotuba yake kwamba kuna kitengo cha matibabu ya kupandikiza figo kwa wagonjwa walio na matatizo ya figo. Hivyo basi naipongeza Serikali pamoja na Waziri wa Afya kwa mafanikio haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kujua mgonjwa anapopata tatizo hili anapata wapi figo hizi kwa ajili ya kupandikiza? Anakuja na mtu wake ambaye atatoa figo au ananunua? Naomba Serikali watupatie majibu ili tuelewe kwa sababu hili jambo limetufanya tupate faraja kubwa.