Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. STELLA A. IKUPA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana pamoja na Naibu wake kwa kuchapa kazi na jinsi wanavyojitoa kuhakikisha afya za Watanzania zinakuwa salama (ulinzi wa nguvu kazi ya Taifa letu). Pili, niwapongeze watendaji wote wa Wizara hii wanaowasaidia Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kutekeleza majukumu yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi; utambuzi wa watu wenye ulemavu wenye vipato duni ili waweze kupatiwa vitambulisho kwa ajili ya matibabu tofauti na ilivyo sasa ambapo mtu mwenye ulemavu mpaka apatiwe barua ya utambulisho. Madhara ya barua ya utambulisho ni pale mtu mwenye ulemavu anapougua ghafla usiku ama akapatwa na ugonjwa akiwa nje ya eneo linalomtambua.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu kuwa Wizara iliangalie hili na ikiwezekana zoezi hili liende sambamba na zoezi linaloendelea sasa la kuwapatia vitambulisho wazee.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema jambo tajwa hapo juu, naunga mkono hoja hii ya hotuba Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.