Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi hii ya kuchangia kwa maandishi. Nitumie fursa hii kuikumbusha Ofisi ya Waziri Mkuu juu ya ahadi yake ya shilingi milioni 10 aliyotoa kwa ajili ya zahanati ya Maligisu alivyokuwa kwenye ziara Wilayani humo.

Aidha, nichukue nafasi hii pia kumkumbusha Waziri wa Afya ahadi yake ya kuongeza vitendea kazi katika Hospitali ya Sengerema, wagonjwa wanapata shida sana pale wanapolazwa ukizingatia hospitali hii inahudumia wananchi wengi wa Wilayani hapo pamoja na mikoa mingine kama Geita na Kigoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.