Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na kuhusu uhaba mkubwa wa watumishi wa afya; kutokana na jiografia ya Visima vya Ukerewe upatikanaji wa watumishi ni tatizo kubwa na hivyo kusababisha vifo vya mara kwa mara hasa mama wajawazito na watoto. Muda mfupi Kituo cha Afya cha Buisya kitakamilika lakini hakina wataalam wa kutosha ili kituo hiki kiwe na ufanisi. Watumishi sita pekee kwa kituo kama hiki ni jambo lisilo na afya. Hivyo, tunaomba watumishi wa afya wenye utaalam kwa ajili ya Kituo cha Afya Buisya na Ukerewe nzima kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, huduma ya afya kwa wazee; pamoja na Sera ya Afya kwa Wazee kutaka vitambulisho kutolewa bure kwa wazee bado wazee (hasa Wilayani Ukerewe) wamekuwa wanatozwa shilingi 1,000 ili kupata vitambulisho hivyo. Naomba Serikali itoe maelekezo/ kauli katika hili jambo ili kuepusha manyanyaso kwa wazee hawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uimarishaji wa Hospitali ya Wilaya; kwa kuwa Hospitali ya Wilaya ya Nansio (Ukerewe) ndiyo Hospitali ya Rufaa kwa Visiwa vya Ukerewe lakini hospitali hii ina upungufu mkubwa wa madaktari pamoja na vifaatiba jambo ambalo limekuwa linaathiri sana utoaji wa huduma kwa wananchi wa visiwa hivi vya Ukerewe. Naomba hospitali hii iangaliwe kwa namna ya pekee kuhakikisha kuwa afya ya wananchi wa Visiwa vya Ukerewe inawekewa mazingira salama.