Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipanafasi hii. Kwanza naomba nianze kwa kuipongeza Serikali kwa kazi kubwa ambayo inafanya hususani kweye mambo ya usambazaji wa dawa, lakini pia nichukue nafasi hii kumpongeza sana Waziri wa Afya, Mheshimiwa Ummy kwa kazi kubwa ambayo anaifanya, sisi wote Watanzania tunaiona, tunakupongeza sana na kama mwanamke tunajivunia wewe kuwa hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumpongeza Naibu Waziri wa Afya kwa kazi kubwa wanayoifanya ambapo wanazunguka na kuangalia ni sehemu gani kuna changamoto, lakini pia na kuendelea kutatua hizo changamoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi hizo, naomba sasa niongee changamoto ambazo zinalikabili Jimbo langu. Jimbo langu mwaka 2016/2017 lilikuwa lina watu 773,000; Jimbo langu lina kata 13 lakini mpaka sasa hivi Jimbo langu halina kituo cha afya. Najua haya mambo yako TAMISEMI Mheshimiwa Ummy, lakini naliongelea kwako kwa sababu wewe ndiye unayeangalia sera, na sera yetu ya afya inasema kila kata iwe na kituo cha afya na kila kijiji kiwe na zahanati.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi watu wa mijini hatuna kijiji, tuna mitaa. Kwa hiyo, nilikuwa nakuomba sana Mheshimiwa Ummy, Jimbo la Segerea, nilisimama mwaka 2016 na 2017 nikiongelea usimamizi wa sera, tunahitaji tupate kituo cha afya. Kutoka kata ya Kisukulu mpaka Amana ni kilomita tisa, kwa hiyo, wananchi wanapata shida sana. Unaweza ukaangalia kwamba labda kwa sababu sisi tunakaa mjini ndiyo maana; labda kwa sababu kuna hospitali nyingi ambapo wananchi wanaweza kutibiwa, lakini ujue kwamba tuna changamoto moja kwamba mtu anapotoka sehemu ya mbali kwenda Amana kwanza kuna foleni ya magari, lakini pia kuna changamoto nyingine ni za mrundikano wa watu kwa sababu watu wote wanakwenda Amana, ni kwa sababu hatuna kituo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na Mheshimiwa Waziri mimi katika Jimbo langu, mfano, kama ukiongelea kata ya Vingunguti ina watu 200,000 na mpaka sasa hivi haina kituo cha afya wala zahanati yake pia haina miundombinu mizuri. (Makofi)

Kwa hiyo, nilikuwa nakuomba Mheshimiwa Ummy, Mheshimiwa Waziri na Wizara yote ya Afya muangalie vizuri Jimbo la Segerea, msimamie hizo sera ili tuweze kupata kituo cha afya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nimeshafanya na Naibu Waziri tumekwenda kata ya Segerea, tukaenda kata ya Mnyamani. Halmashaauri ya Manispaa ya Ilala imeshatoa fidia kwa nyumba ambazo zilikuwa zinaizunguka Hospitali ya Plan International kwa ajili ya kupanua kile kituo ili kiweze kuwa kituo cha afya. Tumeshafanya hivyo, Mkurugenzi tayari ameshatoa hela sasa tunawasubiri ninyi Wizara ili muweze kutuboreshea sasa na kukipandisha hadhi kiwe kituo ili wananchi wanaokaa Jimbo la Segerea wasiweze kwenda Amana au wasiwe kwenda sehemu zingine waweze kuishia pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo nilitaka kuongelea suala la delivery kits ambalo wajumbe wengine waliweza kuliongelea. Mambo ya uzazi ni mambo ya baraka lakini pia ni mambo ya maumbile na pia ni mambo ya majaliwa. Kwa hiyo, nilitaka niongee na Mheshimiwa Waziri, na kwa sababu Mheshimiwa Waziri ni mwanamke najua atalifanyia kazi. Kuna watu wengine ambao wako vijijini akina mama wenzetu hawawezi kununua kwa shilingi 22,000 au shilingi 25,000. Sasa nilitaka niiombe Serikali waangalie wanaweza kuwasaidiaje akina mama wenzetu ambao wako kijijini ambao hawawezi kutoa hizo fedha ili waweze kupata hiyo delivery kits.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tunakuomba sana Mheshimiwa Waziri uweze kunaangalia. Tunajua kwamba lazima na sisi wananchi lazima tuweze kuchangia kiogo katika Serikali lakini pia lazima tuangalie na wananchi wenzetu ambao wanakaa nje ya mijini kwa sababu sisi wa Mijini pengine tunaweza tukawa tuna hizo pesa za kutoa ili tuweze kuangalia.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja.