Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia fursa hii ili na mimi niweze kuchangia hoja hii muhimu sana ya Wizara ya Afya, kwa sababu wote tunaamini kwamba hakuna Taifa lolote linaweza kuendelea bila afya na hata viwanda tunavyotaka kwenda kuvijenga kama Watanzania watakuwa na afya mgogoro ni matatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Wabunge kazi yetu kubwa ni kuishauri Serikali, lakini jambo ambalo linasikitisha sana kazi kubwa pia ya kwetu ni kupitisha bajeti/ kuidhinisha bajeti, tukiamini kwamba bajeti tunayoipitisha inaenda kufanya kazi yake vizuri. Lakini ni jambo la kusikitisha sana kama tunaweza kupitisha bajeti ya maendeleo mwaka jana tulipitisha shilingi bilioni 785 lakini cha ajabu fedha za ndani ukiangalia ni asilimia 17 tu zimeweza kwenda. Kati ya hizo ni shilingi bilioni 64 tu ndani zimeweza kwenda sawa na asilimia 17.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hilo tunawezaje kusema kweli afya zetu zitaboreka. Katika hilo tunawezaje kwenda kusema kwamba hospitali zetu zinaboreshwa, vifaatiba vinanunuliwa, haiwezekani na wala haiingii akilini. Kwa hiyo, naona saa nyingine kwamba hakuna hata sababu ya kupitisha bajeti kama bajeti tunazozipitisha hazitoki hela zinakuwa kwenye makaratasi, lakini uhalisia hakuna, yet Bunge linatumia fedha nyingi Wabunge wake kwenda kukagua miradi, miradi ambayo hakuna hata shilingi moja tumeweka, nadhani hata hao watendaji wanatuona sisi ni watu wa ajabu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, labda nitakuja kuomba mwongozo kuna sababu gani kweli ya Wabunge kukaa hapa miezi mitatu, tunapisha bajeti ambayo kiuhalisia haiendi kufanya hiyo kazi wala hela hazitoki, hizi hela huwa zinakwenda wapi? Kwa sababu kama TRA wanakusanya..., tunajua kwamba tunatumia recurrent bajeti, lakini haiwezekani hela za ndani ziende asilimia 17.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni suala nzima la afya ya mama na jana Mheshimiwa Kangi Lugola alisema kwamba tuwe na Ilani za CCM, nimejaribu kwenda kusoma Ilani ya CCM. Moja ya mambo ni kupunguza vifo vya watoto soma Ibara ya 85, lakini tunashangaa kama Ilani inasema ni kupunguza vifo na vifo vinaendelea vya akina mama maana yake hatuna sababu ya kusoma Ilani ya CCM labda tusome ya Vyama vingine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukija pia kwenye fedha zilizotengwa mwaka jana zilitengwa shilingi bilioni kumi na mbili na milioni mia moja, mwaka huu wameongeza shilingi milioni mia moja lakini hawajatuambia zile shilingi bilioni kumi na mbili za mwaka jana zilienda chache sana. Ukiendelea kuangalia haya mambo najua Mawaziri wanajitahidi sana lakini wanafanyaje kazi kama hakuna pesa. Kwa hiyo, haya mambo kwa kweli ni kuyaangalia sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tunaongelea wanawake wengi wanavyofariki, lakini sijajua nchi hii tumerogwa na nani, mimi naamini aliyetuloga ameshakufa na huko alikozikwa hatujui twende tukafanye matambiko. Leo Tanzania asilimia 70 ya Watanzania ni wakulima lakini tunaambiwa kila dakika 12 mtoto mmoja anafariki kwa sababu ya lishe. Nimepiga mahesabu kama mtoto mmoja anakufa ndani ya dakika 12 ina maana kwa sasa moja wanakufa watoto watano, kwa mwezi mmoja watoto 3,600, kwa mwaka watoto 43,000 kwa uhai wa Bunge miaka mitano ni watoto 219,000. Hili ni janga la Taifa na ninadhani lazima kuwe na mkakati maalum wa kuhakikisha kwamba watoto wanawekewa lishe. (Makofi)

Mimi nina dakika kumi. Mheshimiwa Naibu Spika, twende kwenye suala la Wazee najua halijazungumzwa kwa sababu Wizara hii ni kubwa. Mimi nina declare interest kwamba ni Makamu Mwenyekiti wa Wazee Taifa wa Chama changu, kwa maana hiyo nina kila sababu ya kuzungumzia matatizo makubwa ya wazee.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka Serikali ituambie mwaka 2003 walipitisha Sera ya Wazee, kila nikisimama kuhusiana na masuala ya wazee nazungumzia huwezi kuwa na sera kama hatuna sheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2017 walikuwa na mkakati wa kufuatilia mauaji ya wazee, kama tungekuwa na Sheria ya Wazee maana yake ni kwamba haya mambo yangekuwa yamewekwa na vifo vya wazee vingepungua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wote tunajua kwamba ni wazee watarajiwa, lakini wazee wa Taifa hili wameendelea kuishi kwa matatizo makubwa. Mlizungumzia kwenye ilani yenu kwamba wazee watapatiwa bima na kwamba watakuwa wanatibiwa bure kwenye vituo vya afya. Ninaisoma, Ilani ya Chama cha Mapinduzi Ibara ya 85(h) inasema; “Kuimarisha huduma za matibabu ya wazee nchini kwa kuwapatia vitambulisho na kuwatungia sheria matibabu yao ya bure ili waweze kutibiwa bure katika vituo vyote bila usumbufu wowote.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa kiasi gani mmetekeleza hili? Wazee wanapata matatizo makubwa sana, wazee wanadharaulika hawana hata hivyo vitambulisho, kama wanavyo ni wachache sana. Hii ndiyo Ilani yenu ya 2010/2015 hamjaitekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, walisema kwenye ilani yao kwamba watanunua magari 10 kwa vituo 10 vya wazee; mtuambie ni vituo vingapi vya wazee hapa nchini vimepata magari?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nizungumzie kuhusu suala la matatizo ya afya ya akili (Generalize Anxiety Disorders). Kwa Jiji la Dar es salaam mwaka jana watu 150 mpaka 200 walikuwa wana-report kwenye vituo kwamba wana matatizo ya afya ya akili, hiyo ni kwa Dar es Salaam, ina maana tatizo hili linaendelea kukua kutokana na hali ngumu ya maisha, kutokana na wasiwasi, hawajui kesho yao itakuaje. Hata hivyo hatuna wataalam wanaoshughulika na afya ya akili.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba tuna hospitali kubwa ya Mirembe, tumewahi kwenda kutembelea pamoja na Kamati yangu matatizo ni makubwa sana, watalaam ni wachache sana. Hata hivyo pamoja na kwamba watalaam hawa wachache bado Serikali haijaona umuhimu na ndiyo sababu tumeona kwamba tuna tatizo kubwa la watalaam wa afya mabingwa. Tuna upungufu wa takribani mabingwa 500, na hatujaona mkakati wowote wa Serikali kuhakikisha kwamba tulikuwa na mabingwa hawa ili waweze kusaidia watu wetu. Leo tunapita barabarani tunaona watu wanatembea hawajielewi, Serikali ina mkakati gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna hili suala la kwenda kutibiwa nje, na kwenda kutibiwa nje kuna process ndefu kama ambavyo hata Mheshimiwa Spika amesema hata wengine tumewahi kwenda nje. Hainiingii akilini, juzi nimemsikia Mheshimiwa Waziri wa Afya akizungumza na nitaomba baadae atupe majibu wkaati aki-wind up; anasema kwamba lazima uhakiki ufanyike, mimi nakubaliana naye. Hata hivyo anaposema yawezekana watu wengine wamekwenda tu kufanya plastic surgery; kubadili maumbile au kuongeza maumbile au kufanya vyovyote vile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napata shida sana, kwamba inawezekana hawa wanaokwenda kufanya hivyo hawakupita katika utaraibu wa kawaida, ni vigogo. Mimi ninaamini wananchi wa Tanzania mpaka upate kibali cha kwenda nje ni hassle kubwa sana, lazima jopo la madaktari likae, waangalie, wajue ni ugonjwa gani. Sasa mimi ninaposikia Waziri anasema wengine wamekwenda kufanya mambo mengine ambayo ni kinyume mimi nashindwa kuelewa, na nitaomba aje atuambie ni kwa sababu gani na wizara yake imefanya nini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu masuala ya ukatili wa kijinsia. Ni jambo la kusikitisha kwamba Fungu 53 ambalo ndilo la maendeleo ya jamii limepewa shilingi bilioni 4.9 tu; na mimi nadhani huku ndiko kwenye maafisa ustawi wa jamii nashani na ndiyo sababu hawa maafisa ustawi wa jamii imeshindikana sasa kazi hizo wapelekwe kwa Makonda kule Dar es Salaam na matokeo yake ndiyo haya. Kwamba wizara imeshindwa kufanyakazi yake vizuri inamkabidhi kazi hiyo Makonda na Makonda hana watalaam. Kwa hiyo, ninaomba sana Wizara hii fungu namba 53 lipewe fedha ili watoto wetu waweze kuthaminiwa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)