Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Anna Joram Gidarya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ANNA J. GIDARYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mimi naomba nijikite kwenye hoja iliyoko mezani.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja iliyoko mezani inaonesha kwamba Watanzania ni jinsi gani akili zetu zinachezewa. Bajeti ya Wizara kwa mwaka 2018 inaonesha ni trilioni 1.7 lakini ya mwaka huu ni shilingi 886,236,000,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, unawezaje kuhudumia Watanzania kwa bajeti hii, nchi ambayo watu wake hawana afya nzuri, hawana lishe bora, ni nchi ambayo watu wake kiuchumi na kiafya hakutakuwa na nguvu kazi ya Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inajinasibu kwamba wanafanya mambo mazuri, ni kweli upande mwingine kuna mambo yanaenda sawa. Kuna mambo hayaendi sawa, kwenye Idara ya Afya kuna mambo ambayo tunaona ni kama mchezo wa kuigiza kila mwaka. Issue ya watumishi kwenye hii idara ni issue ambayo imezoeleka, Wabunge wanaleta maswali ya msingi, majibu ya Mawaziri inaonyesha ni kutuchezea akili za Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda kwenye kitabu cha Kamati, TWAWEZA wameleta takwimu inaonesha kwamba kila baada ya dakika 12 mtoto mmoja wa Kitanzania anapoteza maisha kwa sababu ya kukosa lishe. Ukienda tena zaidi wanasema mpaka masaa ya jioni ni watoto 35 wanakufa kutokana na lishe duni, sasa tunajiuliza hii bajeti mmepunguza kwa nini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni idara nyeti, hakuna msomi anayesoma kama hana lishe bora. Hakuna mtu yeyote anayeweza kwenda kwenye Serikali ya viwanda kama hana lishe bora. Tusileteane maigizo ambayo yanaweza yakaleta hasira kwa Watanzania, tunahitaji Watanzania wenye afya njema, tunahitaji Watanzania wenye akili ambazo zina afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna habari ya matibabu bure kwa wazee. Nakubaliana ni kweli kuwe na matibabu bure kwa wazee lakini Serikali haikuangalia ni wapi mtu anapokuwa na magonjwa ya kudumu. Unapokuwa kijana kuna magonjwa si nyemelezi, lakini umri unavyozidi kukua na unapozidi kuzeeka mwili unapoteza nguvu. Kuna watu wanaumwa magonjwa ya figo, kuna watu wanaumwa magonjwa ya tezidume, haya mambo yote yana-compare kwenye uzee, kwenye umri mkubwa, lakini suala la matibabu bure kwa wazee ni paracetamol kwenye vituo vya afya. Kwa namna moja au nyingine tunawapoteza wazee wengi kwa sababu ya huu mwamvuli wa matibabu bure.

Tunaomba sasa mje na mkakati mwingine namna ya kuokoa maisha ya wazee wa Kitanzania ambao wamefikia umri mkubwa na wana mashambulizi ya magonjwa ya kudumu ni mengi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye zahanati zetu kuanzia ngazi ya vituo, zahanati zimejengwa kwa mahitaji ya mtu kama mimi ambaye sina mahitaji maalum. Hawa watu wenye mahitaji maalum hawajawekewa kipaumbele kwenye zahanati zetu, ninategemea Waziri atakapokuja hapa atuambie ana mkakati gani wa kujenga maeneo katika zahanati yetu kwa ajili ya watu wenye mahitaji maalum. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna eneo lingine ambalo ni eneo nyeti, matumizi ya madawa ya kupunguza makali ya VVU, matumizi haya mna…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)