Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Rev. Dr. Getrude Pangalile Rwakatare

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MCH. DKT. GETRUDE P. RWAKATARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi. Naomba awali ya yote nimshukuru Mungu, Baba yetu wa Mbinguni ambaye ametuazima uhai, anatupa afya njema na tuko Bungeni kwa furaha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee kabisa niwadhibitishie kwamba ndani ya Bunge mna Bishop, ndani ya Bunge mna Mchungaji ambaye haachi kuomba kwa ajili ya Spika, Naibu Spika, Wenyeviti wote na Bunge zima; wa CCM na hata Wapinzani, wote ninawaombea Mungu awape kibali kwenye Majimbo yenu kwa jina la Yesu. Namwomba Mungu awape afya njema katika Jina la Yesu. Naomba
Mungu awape maneno matamu, kila mnalolisema liwe sukari masikioni mwa wasilizaji. Yaani mwende kifua mbele kwa kibali kwa wanaume na wanawake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee kabisa napenda nitoe shukrani za dhati kwa Rais wangu kipenzi, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ambaye ameniteua na leo niko Bungeni pamoja nanyi. Mungu ambariki, ampe maisha marefu. Tunapongeza kazi anazozifanya mpaka nchi jirani wanatetemeka. Kwa kweli ni mtu mwema, ni jembe, yeye hakika ni bulldozer, anafanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende moja kwa moja kwa mwenye dhamana ya Wizara hii. Namshukuru kipekee kabisa na nimpe pongezi nyingi Mheshimiwa Ummy Mwalimu kwa kazi nzuri unayoifanya. Wanawake wenzako tunajivunia. Kwa kweli hujatuaibisha. Kila kitu unafanya kwa umakini.

T A A R I F A . .

MHE. MCH. DKT. GETRUDE P. RWAKATARE: Mheshimiwa Naibu Spika, naikataa ila namwombea, Mungu amsaidie.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kipekee kabisa nimshukuru Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na wasaidizi wake wote. Tunasema mabadiliko makubwa tunayaona, asiyekuwa na macho shauri yake. Ukweli tumeona kwamba huduma zilizokuwa zinapatikana nchi za nje, sasa hivi zinapatikana hapa hapa Tanzania, umejitahidi. Siyo hivyo tu, upatikanaji wa dawa sasa hivi ni 85% na bado unasema utaongeza zaidi. Jamani, uimarishaji wa huduma katika vituo vyetu vya afya na hospitali, tumeona huduma za afya zimeimarika kwa kiwango kikubwa sana, tunashukuru na kwa sababu muda wangu ni mfupi, ningependa tu niende moja kwa moja kwa kile ambacho ningependa kuchangia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia kuhusu kinga, tiba bila malipo. Magonjwa mengi yanayotupata Watanzania kwa sababu wengi wanakosa elimu ya kutosha. Nilikuwa naomba tuongeze, kwa mfano, UKIMWI; UKIMWI ni ugonjwa ambao unaweza kuepukika. Tuombe viongozi hata wa dini kwenye mahubiri yao waongeze juhudi ya kuweza kuwaambia watu, wanandoa waweze ku-stick na rafiki au na mke mmoja ambaye ataweza kumsaidia, yaani kama Waebrania 13:4 inasema: “Ndoa iheshimiwe na watu wote, malazi yawe safi.”

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. DKT. GETRUDE P. RWAKATARE: Mheshimiwa Naibu Spika, naipokea. Ni nzuri na ninaombea. Awalete wengi niwaombee wapone, Mungu yupo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nasema kwa habari ya kitabu cha Waebrania 13:4, “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, malazi na yawe safi, washerati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu ya magonjwa yasiyotibika.” Magonjwa yasiyotibika ni UKIMWI na mwengine. Kwa hiyo, kama mtu akiweza kukaa na mke wake bila kwenda mchepuko au nyumba ndogo, uhakika watampendeza Mungu, lakini zaidi sana watajikinga na magonjwa. Watalea watoto wao, kifo ndiyo kitawatenganisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja mia kwa mia