Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii ya Afya. Kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Rais wetu na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi nzuri wanazozifanya. Kwa kweli suala la afya sasa Tanzania tumefika mbali sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Ummy, wewe ni Jembe. Kwa kweli unatosha. Hukuchaguliwa kimakosa katika nafasi hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende moja kwa moja kwa kuipongeza na kuishukuru sana Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kwa kusikiliza maoni ya Wabunge wao na hasa kwa kunisikiliza mimi Mbunge wa Wanawake wa Mkoa wa Mara na Mbunge ambaye ni Rais wa Wabunge wote wa Mkoa wa Mara. Kwa kuwa niliongelea suala la Hospitali ya Rufaa ambayo ni Hospitali ya Kwangwa, kwa kweli nilipoingia tu Bungeni niliongelea na baada ya kuongelea sasa tupo kwenye bajeti. Kwa kweli nami katika Mkoa wa Mara nitaandikwa kwenye wino wa dhahabu. Nashukuru sana kwa hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia namshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuniamini, ananiona ni Mbunge ninayefaa na kutosha ndiyo maana nakuwa mwakilishi mzuri Mkoa wa Mara, amekuwa akinipa vifaa ambavyo nimekwishapeleka katika Wilaya za Bunda, Tarime, Serengeti, Rorya na Wilaya nyingine. Kwa kuwa wale wananchi wanaponituma mimi nafanya kweli, ndiyo maana Mheshimiwa Rais ananiona kupitia kwa Mheshimiwa Ummy. Kwa kweli ninajisifia kwamba ninatosha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba suala lingine, namwomba Mheshimiwa Waziri Ummy aangalie sana sasa suala la zahanati zilizopo kwa Mheshimiwa Getere ambaye sasa naye anatakiwa apate huduma hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza sana Serikali yangu kwa sababu inawahudumia sana Wapinzani. Majimbo yote iliyopeleka vifaa ni ya Wapinzani. Sasa na hili Jimbo la Mheshimiwa Getere jamani ambalo halina kitu chochote ambalo ndiyo la CCM, chama kilichopo madarakani sasa na lenyewe lipelekewe vifaa kwa sababu halina vifaa katika zahanati zake zote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, kuna zahanati ya Hunyali ambayo aliifungua Waziri Mkuu, haina vitanda, mashuka na kadhalika, ambapo vyote hivyo Mheshimiwa Rais alinipa kupitia Mheshimiwa Waziri Ummy na nikavipeleka kwenye Majimbo ya Wapinzani ambayo ni Bunda, Tarime na Serengeti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwenye hiyo zahanati ya kwa Mheshimiwa Getere katika Kata ya Kihumbu kuna hospitali ambayo inatakiwa finishing ambayo ni madirisha na milango. Mheshimiwa Ummy nakuomba uandike tafadhali, nina imani unanisikiliza. Pia kuna dispensary ya Hunyali, kipekee naomba Mheshimiwa Waziri aichukulie kwa umuhimu zaidi kwa sababu jiwe la msingi aliweka Mheshimiwa Waziri Mkuu wetu ambaye ametoka kule siku siyo nyingi sana. Sasa Mheshimiwa Ummy akimaliza tu kwenye hii Wizara yake, nina imani kabisa nitapeleka hayo mashuka na vitanda kwa maana sasa hivi bajeti imekaa sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naishukuru sana Serikali yangu kwa kweli iko vizuri inafanya kazi nzuri. Kwa kweli tumetoka kwenye asilimia 50 mpaka sasa hivi tuko kwenye asilimia 98, anayebisha simuoni wala. Kwa hiyo, naishukuru sana Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kwa kazi nzuri wanazozifanya na hasa Mheshimiwa wetu Dkt. John Pombe Magufuli kupitia jembe lake la ukweli Mheshimiwa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)