Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikushukuru kunipa nafasi niweze kuchangia bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka 2018/2019.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze na pale nikikumbuka bajeti ya mwaka jana nilimwomba Waziri kuhusu hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa, ina upungufu wa Madaktari Bingwa sita. Kutokana na msongamano wa wagonjwa wanaopata ajali kutokana na njia kuu inayounganisha nchi yetu ya Tanzania na nchi jirani Zambia, Msumbiji, Malawi na Kusini. Hata hivyo, hadi tunafikia bajeti hii ya mwaka 2018/2019, sikuweza kusaidiwa hata kupata Daktari mmoja Bingwa wakati aliniahidi hapa. Naomba atakapokuja kuhitimisha aweze kunipa hilo jibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, imeonekana katika Taifa letu saratani ya shingo ya kizazi imekuwa ni tatizo kubwa sana.

Kwa taarifa ya yeye mwenyewe Waziri ameliambia Taifa kwamba katika wanawake wanaopimwa kwa mwaka wanawake 670 hupatikana na tatizo hilo. Hilo tatizo limeonekana ni kubwa na limeonekana kisababishi ni wanaume ambao hawajatahiriwa, lakini sikuona kwenye kitabu chake mkakati ambao ameuweka wa makusudi kutoa elimu kwa kundi la wanaume kutoruka njia mbili ili tatizo hili liweze kupungua kwenye Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka Waziri anapokuja kuhitimisha hoja hii aniambie Wizara imejipangaje kufanya utafiti wa kujua chanzo kikuu kabisa cha kusababisha hili tatizo likue kwa kasi katika Taifa letu kwa maana najua huwezi kutoa tiba kwenye tatizo ambalo chanzo chake hukijui. Ukilinganisha na taarifa ya wataalam hebu turudi miaka ya nyuma tulikuwa na wanaume wengi sana ambao hawajatahiriwa lakini hili tatizo halikuwa kwa kiasi kama ambaccho tunakiona kwa sasa. Hivyo, niiombe Serikali tatizo hili walilogundua ni sehemu moja ndogo tu, sehemu kuu ipo, hivyo Wizara ijipange kufanya utafiti wa kina ili tuweze kutatua tatizo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitakuja kwenye mabadiliko ya tabianchi, sasa hivi katika Taifa letu kumekuwa na magojwa mengi sana ya mlipuko ambayo yanapelekea Taifa letu liweze kutafuta dawa katika nchi mbalimbali kuokoa maisha ya Watanzania. Hata hivyo, inasikitisha sana katika Taifa letu la Tanzania hadi sasa tunapozungumza asprin tunaagiza Kenya, nchi yetu ya Tanzania Wizara ya Afya asilimia 50 inatumia fedha hizi kuagiza dawa nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kitabu hiki hakuna mkakati wa Wizara ya Afya ulioonesha kuwa tunakuja na mpango mbadala kutafuta wadau waweze kujenga kiwanda cha dawa katika nchi yetu ili kulipunguzia Taifa kutumia gharama kubwa sana kuagiza dawa nje ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, inaonekana kwenye Wizara hii kuna 1.5 imepotea, sasa hili ni jambo la kushangaza sana na linasikitisha pale tunapokwenda kwenye hospitali zetu za rufaa kukosa vifaa wakati kuna hela zinazopotea bila kuelewa kitu chochote. Naomba Waziri mwenye dhamana wakati wa…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)