Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia kwa dakika tano. Naomba nianze na kitu kilichotokea hapa wakati Waziri anatoa kauli. Mimi naona mnatu-confuse kwa sababu gani? Tulitegemea kwamba majibu aliyoyatoa Waziri angeyapeleka kwa CAG afute hoja. Mnachotaka kutuaminisha hapa, mimi naaminai kwamba CAG anafanya kazi kwa kupewa vielelezo, kama hakupewa vielelezo Naibu Spika ataandika kitu alichokiona.

Naomba nijadili sasa mambo machache kwa sababu ni dakika tano kwanza nianze na utoaji dawa katika hospitali. Dawa zipo, ninachotaka kuongelea ni namna wale Wafamasia wanavyotoa dawa kwa wagonjwa. Wafamasia wanatoa dawa kwa wagonjwa bila kutoa maelekezo ya kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, ziko dawa ambazo ukisoma leaflet yake ukishapewa dawa wanakwambia kwamba labda hii dawa unapaswa uiyeyushe kwenye maji kabla ya kumeza au utumie hiyo dawa kabla ya kula au masaa fulani kabla ya kula au hizi dawa zinaendana na chakula. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kinachotokea Wafamasia wetu wamekuwa wakitoa dawa hizo kwa kuonesha kwamba unatumia moja mara moja, mbili mara tatu na kadhalika bila kutoa maelekezo ya kutosha kwa wagonjwa. Kwa hiyo, unakuta wakati mwingine mtu anakwenda kumeza dawa ambavyo haitakiwi na kwa kweli haileti tija katika matibabu yake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee kuhusu uzazi wa mpango, Mheshimiwa Waziri nimepitia kitabu chake hicho ameandika maneno mazuri na anafanya kazi sio mbaya, lakini hakuna mahali alipogusa kuhusu uzazi wa mpango. Huku nyuma kulikuwa na kitengo wakati wa Awamu ya Kwanza kulikuwa na kitengo kinaitwa UMAT (Uzazi na Malezi Bora Tanzania).

Mheshimiwa Naibu Spika, kitengo hiki kilikuwa kinafundisha mambo mengi kutumia dawa ya kinga ya kuzaa, kufundisha wanawake namna ya kujitunza, namna ya kulea watoto wao na namna ya ku-space ili wasizae watoto wengi na kwa wakati muafaka. Kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Waziri, kitengo hiki hata kama hakitarejeshwa kama kilivyokuwa, lakini wkiangalie ili kiweze kwenda kutoa elimu ya kutosha kule chini kwa wanawake wa vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nije sasa kwenye lishe, ukienda kwenye ukurasa wa 89 wa kitabu chake, Mheshimiwa Waziri ameongea kuhusu lishe, ameongea mambo mazuri ambayo yanahusu mashirika mbalimbali namna ya kurutubisha vyakula ambavyo tunakula, kuweka madini ya joto na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, namshauri Waziri kwamba lishe ndio msingi wa maisha ya mtu katika kukua kwake kimwili na kiakili. Kwa hiyo, ni vyema hiki kitengo cha lishe na taasisi hii iwe mtambuka, washirikiane na Wizara ya Kilimo pia na Idara ya Maendeleo ya Jamii . (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wako hawa Social Workers ambao kazi yao ni wataalam wazuri kabisa wa kutoa ushauri kuhusu mambo hayo lakini hawaajiriwi, wanafundisha watu kila siku lakini hawapewi ajira na hawa watu wa muhimu sana katika maendeleo ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.