Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia. Kwanza niungane na wenzangu kuipongeza Serikali inayoongozwa na Dkt. John Pombe Joseph Magufuli pamoja na Mawaziri wote pamoja na Waziri mwenye dhamana ya Wizara ya Afya na watendaji wake wote, Makatibu Wakuu na kadhalika. Kazi ambayo inafanywa na Serikali hii hakuna mfano, ni kazi nzuri sana ukienda kwenye idara na wizara mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nichangie hii moja tu ya afya. Katika halmashauri yangu ya Mji wa Makambako tumepewa fedha shilingi bilioni moja milioni mia tano kwa ajili ya kujenga hospitali yetu ya Mji wa Makambako. Tumepewa shilingi milioni mia saba kwa ajili ya kuboresha kituo chetu cha afya katika Kata ya Lyamkena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu kwa Serikali, naomba sana katika hospitali au kituo kilichopo Makambako pale; pale ni centre. Dawa tunazopata hazikidhi, tunahitaji tuongezewe dawa ili ziweze kuhudumia watu wetu; na ndiyo maana na mimi nimeunga mkono jitihada za Serikali zinazofanywa na nimejenga vyumba viwili vya Madaktari pale vitafunguliwa mwishoni mwa mwezi huu, vyumba viwili vya kutolea huduma vya Madaktari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wanazungumza; Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi amewahi kusema kwamba Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi kubwa aliyofanya kwa miaka miwili katika sekta mbalimbali ni sawa na miaka 10, hakuna mfano. Sasa kwa kazi hizo ambazo anazifanya; ukienda kule China Rais wa China amepewa kuwa ni Rais wa maisha kutokana na kazi anazofanya, kwa nini Magufuli asiwe Rais wa maisha kutokana na kazi anazofanya? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa miaka miwili tu kazi ambayo amezifanya ni nzuri na kubwa. Kwa kweli lazima tumuombee kwa Mwenyezi Mungu aendelee kuishi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wako watu hapa kazi yao ni kubeza. Nilikuwa namsikia mtu mmoja akisema hizi hela ambazo zimewekwa hapa kwenye bajeti kama hazitaenda hizo hela basi nipeni mimi. Wako watu hapa wanabeza, jamani hii ni bajeti, ni mwelekeo wa bajeti, lazima tuishukuru Serikali kwa kazi inazofanya. Mnasema kama hizi hela zimewekwa tu, kama haziwezi kwenda; amesema mwenzangu mmoja kule kwa hata unapoamka unasema Mungu wangu tunakuomba na kadhalika; lakini yako mambo unamshukuru na kumwomba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hebu tamka unanijua? (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru sana Serikali kwa kweli kwa kazi nzuri ambazo zinafanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nimalizie, pamoja na dakika chache hizi niiombe sana Serikali; tumejenga zahanati 10, tumeshaezeka, tumepiga lipu, tuko hatua za mwisho. Tuiombe Serikali mtutengee fedha kwa ajili ya kumalizia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, mimi pamoja na Wabunge wenzangu wa Mkoa wa Njombe, tunaipongeza Serikali kwa kutujengea Hospitali ya Mkoa wa Njombe. Jengo la OPD limeisha, ombi langu kuwa fedha zilizotengwa hapa tuone namna ya kumalizia hospitali ile ili ianze kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na Mungu akubariki sana.