Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuchangia mchana huu wa leo. Awali ya yote nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kunipatia afya ya kuweza kusimama mbele ya jukwaa hili. Pia nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na timu yote ya Wizara ya Afya kwa kazi nzuri wanayofanya. Mungu awabariki ana azidi kuwatia moyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakuwa sijatenda haki kama sitompongeza Mheshimiwa Rais, kwa kazi nzuri anayofanya na kwa usikivu alionao. Tumekuwa tukiona maendeleo mbalimbali hata katika sekta hii ya afya katika ugawaji wa madawa na kuyasambaza, pia hata katika usambazaji wa magari ya kubebea wagonjwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda katika hili niseme ahsante sana kwa Serikali kwa ambulance ambayo tumepoke katika Kata ya Kabila, Jumamosi iliyopita imewasilishwa na Mbunge tunashukuru sana, sisi kama wananchi wa Magu tuna imani sana na Serikali hii na kwamba mnatusikiliza na tutazidi kuwa pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi hizo bado kuna changamoto kubwa sana ya ukosefu wa watumishi katika sekta ya afya. Zahanati zetu, hospitali zetu zina changamoto kubwa sana, hivyo basi Serikali iliangalie hili kwa ukaribu kama ilivyotoa ajira hapo nyuma ijitafakari tena itoe kulingana na matakwa halisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na changamoto ya ukosefu ya chanjo kupungua kwa kasi bado kumekuwa na tatizo la chanjo ya kichaa cha mbwa. Chanjo hii imekuwa ni adimu imekuwa kama bahati nasibu, naomba Serikali iangalie kwa ukaribu, kwanza ni gharama kwa mwananchi wa kawaida, sindano moja siyo chini ya Sh.30,000, lakini hata kuipata hiyo sindano inaweza ikawa shida, ikakulazimu kutoka nje ya mkoa. Hivyo basi, tunaomba Serikali iangalie kuanzia bei na upatikanaji wake kwani sindano zinazohitajika ni tatu, kwa hiyo Sh.90,000 kwa mwananchi wa kawaida ni kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nimevaa uhalisia wangu, mimi kama champion wa hedhi salama sitajisikia vizuri kama sitaishauri Serikali siku ya leo juu ya hedhi. Suala la hedhi tumekuwa tukilichukulia poa kwa sababu siyo ugonjwa, ndiyo kweli siyo ugonjwa lakini tatizo la hedhi kutokuwa salama ni changamoto kubwa sana na imekuwa ikisababisha magonjwa mengi mno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri atakubaliana na mimi kwamba dawa nyingi antibiotics wanazosambaza katika vituo vyetu vya afya, katika hospitali zetu zinakuwa consumed na wanawake, wanawake ambao wanatibiwa magonjwa ambayo yanatokana na ukosefu wa hedhi salama, ni lazima tukubaliane na hilo. Ndiyo maana tunasimama hapa na kusema kwamba Serikali iangalie namna ya kuweza kutoa nyenzo za wanawake na wasichana katumia katika siku zao, tunachomaanisha ni kwamba ni bora tu-prevent magonjwa kuliko kuacha yatokee ndiyo tutoe dawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo suala hili ni muhimu sana Serikali kuliangalia, pamoja na kwamba tunafahamu mnayo mambo mengi ya kutekeleza...

T A A R I F A . . .

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea taarifa hiyo kwa niaba ya wanawake wote wa Kitanzania. Kwa hiyo, tunaposema wapewe nyenzo hizi ni kwamba tunataka ku- prevent magonjwa kuliko kutibu na kama tunavyojua prevention is better than cure. Kwa hiyo, tunaamini kabisa Serikali hii sikivu leo hii itaenda kujitafakari upya. Pamoja na kwamba wana mambo mengi tunaamini wanao wadau wengi ambao wanaweza wakawa-aproach wakaweza kuwasaidia katika hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tunafikiria huko, tuangalie pia namna ya kupunguza bei ya hizi taulo za kike tuangalie kuanzia VAT kama zinaweza kufutwa zifutwe, kama kuna possibility ya regulate bei ili wanawake wote na wasichana waweze ku-afford itakuwa ni vema zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo nianze kuchangia masuala yanayohusu mkoa wangu.

Katika Wilaya ya Ukerewe Mkoani Mwanza kumekuwa na changamoto nyingi sana za kiafya, kwa wale ambao hawaifahamu Ukerewe Wilaya hii ni muunganiko wa visiwa 38. Kipo Kisiwa cha Irugwa kina changamoto nyingi kwa nini nimekichagua chenyewe tu katika visiwa vyote 38.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwananchi kutoka Irugwa kuifikia hospitali ya Wilaya anachukua takribani saa nne na kuendelea, siyo kwamba katika kisiwa hiki hakuna zahanati, kisiwa hiki ni Kata pia na ina zahanati, lakini cha ajabu ni kwamba ina mtumishi mmoja tu ambaye ni Mhudumu ambaye hana ruhusa hata ya ku-prescribe nusu ya kidonge cha panado kwa mgonjwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wakati sasa wa Serikali hii kusikilza kilio hiki, wananchi wa Irugwa wameteseka kwa muda mrefu, naomba sana uwepo wa haraka sana wa kuwapatia wafanyakazi wa afya kwa sababu wamekuwa wakihangaika kwenda katika hospitali ya Wilaya na ukizingatia kwamba usafiri waotumia si salama…

T A A R I F A . . .

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kufahamu japo sijaipokea kama ambavyo unataka wewe, kwa sababu nina maana yangu ya kuchangia hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendeleee kusema kwamba usafiri ule siyo salama na kama Serikali imetenga tunashukuru kwa usikivu wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia zahanati hii kuna haja ya kuipanua kuwa kituo cha afya kutokana na wingi wa mahitaji ya wananchi wa pale kwa ajili ya matibabu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Kwimba, Jimbo la Sumve tunashukuru sana kwa ahadi ambayo mmetimiza ya kukitengea kituo cha afya cha Malya milioni 400. Ni mara nyingi Mbunge wa Jimbo hilo amekuwa kipiga kelele na mwaka jana nilimpa support ya kusimama hapa, na kuomba kwamba Serikali iangalie ahadi hizo. Akinamama walikuwa wanajifungulia kwenye sakafu, lakini leo Mheshimiwa Waziri ametufuta machozi, wameweza kututengea milioni 400, tunachoomba sasa ni kutupatia milioni 350 ambayo ni ya kununua vitanda na vifaa vya tiba ili shughuli ziweze kwenda kama ambavyo tulikuwa tunatarajia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.