Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi kuchangia bajeti hii ya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa nafasi hii ya uhai kuweza kuwa mahali hapa kufanya kazi hii ambayo ni kwa ajili ya wananchi. Nitajielekeza moja kwa moja katika kuchangia bajeti hii. Namheshimu sana Mheshimiwa Waziri wa Afya pamoja na Naibu wake lakini katika majibu ya mwezi Mei mwaka 2017 kuna hoja ambazo tulikuwa tukiuliza kuhusu afya ya mama na mtoto na jinsi ambavyo wanaweza wakakinga akinamama kutopata vifo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu haya tuliambiwa kwamba, Wizara na Serikali kwa ujumla imejipanga kuhakikisha kwamba wanapunguza katika vizazi hai 100,000 watafikia wanawake 292 angalau watakaokuwa katika hilo. Hata hivyo, sasa hivi mmeona wanawake katika vizazi hai 100,000 wanaopatwa na vifo ni 556, imepanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hiyo naomba majibu Mheshimiwa Waziri atuambie ni mkakati gani ambao wanaenda kufanya akinamama hawa wasiweze kupoteza maisha yao wakati wa uzazi. Tunaomba mkakati madhubuti wa Serikali ambao utakwenda kupunguza ama kumaliza tatizo hili la akinamama pamoja na kazi kubwa ambayo inafanyika ya kupeleka vifaa na kadhalika nini kilichopo hapo kinachopelekea ongezeko hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ni bajeti kutotoka kwa wakati. Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, kama alivyokwishasema mwenzangu tunatenga bajeti, lakini utekelezaji wake unakuwa ni mdogo sana. Waziri atuambie nini kinafanya hivyo, tumekwenda katika ziara katika Mkoa wa Iringa, tumekwenda Mkoa wa Mbeya, tumeona wenyewe, inafika mahali mnaona aibu kama Wabunge, mnakwenda kukagua miradi ambayo pesa hatukupeleka. Tunawaweka katika mazingira gani hawa Watendaji ambao tunasema tunakuja kukagua pesa ambazo zilitumwa, tuliidhinisha mwaka wa fedha huu wa 2017/2018 halafu mnakwenda pale hakuna hata shilingi moja iliyokwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekwenda Chuo cha Rungemba cha Maendeleo ya Jamii, hakuna fedha iliyokwenda. Tumekwenda Chuo cha Uyole Maendeleo ya Jamii, hakuna fedha iliyokwenda. Tumekwenda katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya ambayo inahudumia mikoa saba lakini hakuna fedha iliyotengwa iliyokwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli wale Wakurugenzi wanafanya kazi kubwa sana. Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya ameweza hata kuajiri wafanyakazi kwa kutumia own source, kazi ambayo ilikuwa ifanywe na Serikali hii lakini amekwenda kufanya hiyo kazi. Tunampongeza kwa sababu wananchi waliweza kupata huduma. Tunaitaka Serikali ipeleke pesa wananchi waweze kupata huduma kama tunavyopitisha bajeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya mwaka 2017/2018 iliongezeka kwa asilimia 35 kutoka bajeti ya 2016/2017, lakini bajeti hii ambayo tunaijadili sasa imepungua kwa asilimia
20. Hii maana yake nini? Ni kwamba tunakwenda kuwahangaisha wananchi tena kule, hawatapata madawa, hawatapata huduma bora inayotakiwa, vifaa tiba na kadhalika, hii inakwenda hadi kwenye Mkoa wangu wa Iringa, ukiangalia Mkoa wa Iringa Wilaya ya Kilolo ambako…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)