Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ili nami niweze kuchangia Wizara hii nyeti ya Afya. Mwaka 2001 African countries kwa maana ya AU na Tanzania ikiwa mmojawapo walisaini convention ya Abuja declaration na wakuu wote wa nchi walikubaliana kutenga angalau asilimia 15 ya bajeti yote ya nchi kwa ajili ya afya, lakini tukiangalia miaka 17 sasa hivi hilo halijawahi kutokea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia bajeti ya mwaka 2017 ukurasa wa nane inaonesha Bunge tuliidhinisha 1.1 trillion lakini pesa zilizopelekwa ni asilimia 57 tu. Pia hii bajeti ya 1.1 trillion ilikuwa ni asilimia 3.5 ya bajeti nzima ya Taifa. Pesa za Maendeleo kwa Wizara ya Afya, pesa zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo, pesa za ndani zilikuwa asilimia 24 tu zilizokwenda ambayo ni almost eight billion na pesa za nje zilienda shilingi bilioni 321 ambayo ni sawa sawa na asilimia 71. Sasa kama tunaweza kutenga pesa kidogo hivyo, kutokana na mapato ya ndani, tunategemea zaidi pesa za nje, hivi kweli tuna nia ya dhati ya ku-improve sekta ya afya? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija kwenye bajeti ya Afya ya mwaka huu, imepungua kutoka 1.1 trillion mpaka 0.9 almost shilingi bilioni 898 ambayo ni pungufu ya asilimia 22. Hivi kweli are we serious? Tunawezaje kupunguza zaidi ya asilimia 20 kwenye sekta muhimu kama ya afya? Hii ni sekta inayo-deal na afya za watu, tunapunguza pesa kiasi hicho! Napenda Mheshimiwa Waziri wakati anakuja ku-wind up atueleze ametumia criteria gani kupunguza zaidi ya asilimia 20 ya bajeti ya Wizara hii? Ni kwa sababu labda changamoto zimepungua au magonjwa yamepungua? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia ukurasa wa 128 pia pesa zilizotengwa kwa ajili ya Fungu 52 - Wizara ya Afya, bado pia ni kidogo sana na asilimia 67 imetengwa kutoka pesa za nje. Tuna guarantee gani kwamba tutazipata hizi pesa kutoka nje, kama sisi wenyewe we are not committed kutoa pesa za ndani kwa ajili ya afya za watu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kuhusu vifo vya akina mama wakati wa kujifungua (maternal mortality rate). Taarifa ya Tanzania Demographic Health Survey ya mwaka 2015/2016 inaonesha vifo vya akina mama wakati wa kujifungua vimeongezeka kutoka akina mama 432 mpaka 556 kwa kila uzazi kwa watu laki moja. Moja ya sababu ni zaidi ya nusu ya akina mama wanajifungulia nyumbani. Pia hiyo taarifa inaonesha ni asilimia 46 tu ya akina mama wakati wa kujifungua wanahudumiwa aidha na daktari au muuguzi au clinical officer. Sasa tuna zaidi ya miaka 50 ya uhuru, I think Serikali ya CCM mmekuwa very comfortable ndiyo maana mnacheza na afya za watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli zaidi ya asilimia 50 ya akina mama wanaojifungua kwenye Taifa hili hawapati huduma wakati wa kujifungua na tunasema tuna nia ya dhati ya kupunguza vifo vya akina mama wakati wa kujifungua, I think we need to be serious. Mheshimiwa Ummy wewe ni mwanamke, wewe ni mama unajua ni jinsi gani mtu anapata shida kubeba mimba miezi tisa halafu anakuja anapoteza maisha au anapoteza maisha ya mtoto wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuomba Mheshimiwa uliangalie hili suala kwa makini kama wewe mwenyewe ulivyoonesha kwenye hotuba yako ukurasa wa saba kwamba mnataka kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025, Mpango wa Maendeleo wa Kati 2020/2021, Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2015/2016 na Sustainable Development Goals (SDG) 2030 ambayo tunataka iwe chini ya akina mama 200 wanafariki wakati wa kujifungua; lakini tunaona trend inaongezeka. Sasa kama trend inaongezeka ndani ya mwaka mmoja, akina mama zaidi ya 100 wamefariki, tunafikiaje hiyo less than 200 mwaka 2020. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa, niwaombe Wabunge wote akina mama zile shilingi trilioni 1.5 zilizopotea, tumwombe na tumuunge mkono Mheshimiwa Rais zipatikane ili tuweze kuboresha na kujenga vituo vya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naomba kuiongelea Hospitali ya Jimbo langu ya Wilaya ya Serengeti. Hatuna hospitali ya Wilaya tangu uhuru.