Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi ya kwanza kwa kuwa mchangiaji wa kwanza katika Wizara hii ya Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda Serikali itueleze ni kwa kiasi gani wanajiandaa kuweza kutenga ile asilimia 15 ya bajeti ili waweze kutekeleza lile Azimio la Abuja? Wasipofanya hivi wanashindwa kutekeleza mambo yao ya maendeleo, wanashindwa kujenga vituo vya afya na kupata vifaa kwa ajili ya hizi hospitali. (Makofi)



Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie KCMC. Napenda niwapongeze sana KCMC, Mheshimiwa Waziri ameeleza kwamba wametibu wagonjwa 1,100 wenye matatizo ya saratani na wanaweza wakafanya vizuri zaidi. Wamejaribu kutafuta wafadhili, wamewafadhili wamepata vifaa vyote vya mionzi na kila kitu wamepata kwa ajili ya ile unit ya saratani. Kinachopungua pale ni lile jengo banker kwa ajili ya mionzi. Wanahitaji karibu shilingi bilioni tano, lakini mnaweza mkawasaidia kwa kuwapa kwa awamu. Siyo lazima muwape yote kwa pamoja. Mkiweza kuwapa hizo fedha kwa ajili ya kujenga ile banker itawasaidia sana kupunguza msongamano katika Hospitali ya Ocean Road.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba yake nimeona Mheshimiwa Waziri anatoa sana fedha nyingi kwa ajili ya Ocean Road, lakini pia KCMC ikisaidiwa, mtasaidia sana hii Kanda ya Kaskazini kupunguza msongamano katika Hospitali ya Ocean Road. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niizungumzie hospitali yetu ya Mkoa wa Kilimanjaro ambayo ni Hospitali ya Mawenzi. Hospitali ile Mheshimiwa Waziri naomba itupiwe jicho. Ni Hospitali ya Rufaa lakini haina Emergency Unit. Tunaomba mhakikishe kuna Emergency Unit na iwe fully equipped, kuwe na timu ambayo inaweza ikahudumia wakati wa emergency.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Hospitali ya Mawenzi haina isolation room. Unakuta mgonjwa ana TB analazwa na mgonjwa mwenye malaria. Sasa mgonjwa mwenye malaria anaenda hospitali kutibiwa malaria akirudi nyumbani anaweza akapata TB. Kwa hiyo, tunaomba sana mtuhakikishie kwamba kunakuwa na isolation room pale Mawenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kile Kitengo cha Wagonjwa wenye Matatizo ya Akili kwa kweli kiko kwenye hali mbaya sana. Wale wauguzi wanafanya kazi pale lakini unakuta saa nyingine hawa watu wenye magonjwa ya akili wanaweza wakawapiga. Sasa kutoka kule kwenye wodi ya wagonjwa



wenye akili mpaka waweze kupata msaada, hamna hata kengele ya kuweza kupiga ili waweze kusaidiwa. Kwa hiyo, unakuta wale wauguzi wana shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo hapo kuna ile rehab ambayo ina-serve kanda nzima ya Kaskazini, lakini ile rehab imesahaulika kabisa, haina uzio, hawapewi hata sabuni, hawapewi vyakula, unakuta watu wanajitolea kusaidia. Sasa nataka kujua hii Serikali mnasema mnawasaidia wanyonge, hapa mnawasaidia wanyonge kweli? Kwa sababu wale wanaoenda kule unakuta wengine hawana hata familia, wamekaa tu pale wameachwa hamna dawa. Ukiangalia madaktari, hawapo wa kutosha. Sasa sijui mna mpango gani wa kuhakikisha kwamba tunapata madaktari wa kutosha katika kada hii ya wagonjwa wenye matatizo ya akili? Kwa sababu nasikia ni madaktari 26 tu nchi nzima tulionao. Sasa kwa mtindo huu, sijui ni kwa jinsi gani mtaweza kuwasaidia hao wanyonge ambao mnasema mnawasaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna upungufu mkubwa wa Madaktari wa Nusu Kaputi. Sijasikia kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri ni kwa kiasi gani mnaenda ku-train hawa madaktari wa nusu kaputi. Napenda Mheshimiwa Waziri wakati anakuja ku-wind up atuelezee ni nini anachoenda kufanya ili tuweze kupata madaktari wa kutosha wa nusu kaputi.

Sasa hivi tumeona kuna mafuriko yametokea katika Mji wetu wa Dar es Salaam na Morogoro. Tunajua mafuriko yakitokea kutakuwa na magonjwa ya mlipuko. Dar es Salaam mafuriko yakitokea watu ndio wanafungua yale ma-septic tank, kwa hiyo, unakuta maji yanachanganyika na vinyesi na tunajua kipindupindu kwa lugha ya sisi ambao sio Madaktari ni kwamba mtu amekula kinyesi. Sasa sijui Serikali mna mpango gani au mmejitayarishaje kuhakikisha kwamba magonjwa ya milipuko yakitokea mnaenda kui-handle namna gani? Kwa sababu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)