Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

MHE. EMMANUEL J. PAPIAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza napongeza Serikali kwa jitihada ambazo imezifanya kutupa huduma pale Kiteto kwa kutujengea kituo cha afya pale Sunya, wanajenga barabara ya zaidi ya bilioni 6.3 kwa kupitia fedha za USAID, niipongeze sana Serikali. Naipongeza Serikali kwa jitihada ambazo zimetupa kwa kujenga shule zetu za sekondari zaidi ya milioni 215 imetuletea na shule inaendelea kupauliwa na sasa vijana wetu wataendelea kupata elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali yetu ya Wilaya ya Kiteto ilikuwa ni kituo cha afya na baadaye wakaamua kiwe hospitali ya Wilaya. Sasa nataka kuomba Serikali itusaidie ikiweza kututengea milioni 500 tukaongeza majengo kwenye ile jengo, hospitali yetu ya Wilaya itakuwa imekamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, tuna jengo la boma la halmashauri ambalo linaendelea kujengwa na hili jengo tumefikia mahali ambapo sasa tuko kwenye hatua za mwisho. Hata hivyo, kwa mwaka huu haikutengewa pesa zozote kwa mwaka wa 2018/2019, hili jambo limetusikitisha sana, tunaomba Serikali iliangalie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe, kuna maeneo ambayo yametengewa pesa kwa ajili ya majengo halmashauri zao hawajenga, hawana viwanja, wanatafuta maeneo, wako kwenye michakato. Pesa zimekaa zaidi ya miaka miwili, lakini kwa halmashauri ambayo ni kama ya Kiteto jengo liko kwenye finishing haliwezi kupata pesa. Niombe Mheshimiwa Waziri Jafo hili suala analifahamu hili jengo amelitembelea afanye jitihada atutengee pesa tumalizie jengo sisi tuendelee kuchapa kazi pale Kiteto. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuomba kuna hili suala la TARURA, barabara vijijini. Niishauri Serikali iangalie upya, hawa ma-engineer hebu wapeni training. Usimamizi wa hizi barabara unatupa mashaka, Mheshimiwa Waziri Jafo ameshiriki kuona ile barabara ya Sunya Namelock na jinsi ambavyo madaraja yamejengwa, tuna Mkandarasi Mshauri Mtanzania amepewa kazi. Madaraja hayawezekani kupitika tu peke yake na hata tu kupitisha maji kwa sababu yale ambayo yamekwishajengwa, Engineers wapo, wataalam wapo, Engineer wa Wilaya yupo, tumehangaika angalia barabara haiwezi kupitika ambayo ina-spend over 6.3 billion, hivi kweli hawa ma-engineer ni Watanzania na wazalendo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe kwenye hili, hii barabara ya Sunya Kiteto Sunya Namelock hii barabara isipopitika, imetumia bilioni 6.3, hawa ma-engineer mshauri wa madaraja, hawa watu naomba Serikali iwashughulikie, kabla ya hapo wasipofanya hivyo, hii barabara isipopitika miaka mitatu ijayo mimi Rais akikanyaga Kiteto ni wa kwanza kushika maiki kutaja hii kampuni ya kitapeli iliyo tapeli Wilaya yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, utawala bora, hebu tusaidieni jamani watu wa utawala bora, hebu kaeni na watendaji wa Serikali wafundisheni zile ethics za zamani tulizokuwa nazo, watu wajue namna gani ya kufanya kazi kwenye maeneo yao. Migogoro mingi inayoibuka kwenye maeneo yetu ni kwa sababu watu wameshindwa kui- manage kabisa na hawahangaki nayo. Niombe utawala bora Wizara ya Mheshimiwa Mkuchika isimame iliangalie hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili liende sambamba na kutoa watumishi. Leo tunajenga vituo nchi nzima vya afya watendaji wako wapi, leo Kiteto pale ina zahanati haina mtumishi dawa wananchi watakunywa wapi, niombe nahitaji watumishi wa afya watumishi waliondoka wote na watumishi wamehamishwa, Wizara ya TAMISEMI imesema mtumishi anapoomba uhamisho apewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa watumishi Kiteto wamehama 30, nina deficit ya 30, nipeni watumishi wangu niendelee kubaki na deficit lakini nikibaki na walewale wa 30. Mmewaruhusu na hamkunipa wengine, sasa watumishi watafanyaje kazi. Niombe Serikali nahitaji watumishi wa Wizara ya Afya, vituo vimefungwa, vimesimama, hakuna mtu mwenye uwezo wa kutoa dawa, wananchi wanakuja vituoni, lakini hawapati huduma. Sasa naomba Serikali iliangalie hili haraka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeomba ambulance zaidi ya miaka mitatu tangu nikanyage hapa Bungeni. Ambulance inayotumika pale Kiteto ni gari ya CCM ambayo nai-service mimi na naweka mafuta na kadhalika. Sasa niambieni hii gari inaenda kuchakaa, sasa kwa nini isipewe gari ya ambulance wakati mnajua maeneo makubwa coverage umasaini pale Makame, Ndedo, Loolera clinic sasa akinamama hawawezi kwenda? Kwa nini akinamama hawawezi kwenda clinic na Wabunge wa Viti Maalum naomba humu ndani mkinyanyuka wa Manyara, mdai gari ya ambulace pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekuwa mpole sana sasa I am too tired! Sasa nasema, ifikapo mwezi wa Nane hamjanipa gari nawapa gari ya Ubunge iende kuchapa kazi kule, mimi nitatembea na daladala. Siwezi ku-tolerate this level kwa sababu wananchi wanajifungulia kwenye magari, wanajifungulia kwenye lori, wanajifungulia barabarani, tunaegesha malori yanashusha kuni wanawake wanajifungua tunawapakia humu, tunaelekea wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiteto coverage kwenye zile rural areas hatuwezi kutembea watakwenda wapi nimekuwa mpole sana sasa imefika mahali I am too tired, nahitaji gari immediately. I am too tired, nahitaji gari la ambulance siyo ya kwangu, nimeomba Ofisi ya Waziri Mkuu, nikamwambia kama kuna gari imeanguka kwake Ofisini wanipe hilo gari nishirikiane na Mkurugenzi tukarabati litembee hakuna.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nikamwambia Mheshimiwa Jafo nipeni gari lililoanguka hapo nishirikiane na Mkurugenzi tutengeneze, hakuna. Sasa nifanye nini? Nataka gari I am tired, nataka gari. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mikopo ya vijana, vijana, vijana wamefungua SACCOS tumehangaika, Mkurugenzi wa Halmashauri amekusanya ile 10 percent, ameingiza 10 million amehangaika, tumehangaika tumechangishana, vijana wameanza kukopa, nimeomba pesa jamani tusaidieni kwenye hii mifuko ya vijana hii mnayoitaja kila siku, haya mabilioni mnayosema, mbona hatuyaoni kule kwa wananchi? Wameomba document tumeleta hapa, SACCOS iko very straight, vijana wapo, wanalima, wanafuga, wanahangaika barabarani, kwa nini hamtupi hata fedha kidogo wale vijana wakafanya kazi, kwa nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii mifuko wanayoitaja ni ya nini? Combine hii mifuko yote, hii mifuko waliyoitaja ya vijana wakusanye kwenye mfuko mmoja, waweke mahali pamoja, waonyeshe data kwamba tumetoa hapa, tumepeleka hapa otherwise hakuna kilichofanyika na mwisho wa siku watakuwa wanasoma takwimu ambazo siyo kweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe SACCOS yangu ya vijana na wanawake wamefungua pale, Mkurugenzi amehangaika nina Mkurugenzi mzuri sana, hizi 10 percent anahangaika nazo, anatoka Ofisini saa saba, saa nane, anakusanya pesa anaingiza kwenye ile mifuko, vijana wanakopa, naomba Serikali im-support, imuunge mkono Mkurugenzi otherwise watakuwa wanamsulubu na vijana wetu hawawezi kufanya kazi, mwisho wa siku tutakuwa na vijana wahuni mtaani tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kushauri, ukiwa unajenga majengo mengi, una-project kwenda kutoa huduma, nenda sambamba na watumishi. Niombe Serikali iwarudishe wale vijana wa Rural Medical Aids, zamani walikuwa wanabeba kits, anakwenda hospitali, zahanati, anakaa hapo, anasubiri mgonjwa, anamtibu, anaendelea sasa rudisheni hawa vijana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa vijana mnawalipa mishahara midogo, mshahara kidogo, kesho anakwenda Medical Assistant, atakwenda RMO eshokutwa atakwenda degree, mwisho wa siku unampandisha polepole na Serikali through the budget itakuwa inakwenda inapanda polepole kuendelea kuwa-accommodate hawa watu, lakini tuwe na watumishi kwenye rural areas ili zile zahanati zetu ziweze kufanyakazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba hawa watumishi warudisheni ili hivi vyuo virudi kufanya training kwa sababu ni vijana ambao walikuwa wana-rescue situation, sambamba na enzi zile mnakumbuka UPE tulikuwa na Walimu wa darasa la saba wanafundisha, leo tumewa-phase out tumemaliza lakini ni we need Teachers. Lazima tuwe na alternative as a Government, lazima tuwe na alternative na options kwenda sambamba, tunajenga shule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maboma mengi kule Kiteto, mengine siyasemi hapa, siwezi kuyasema hapa ni ya kwangu na kifua changu, siwezi kuyasema hapa, lakini niombe; nipeni special funds kidogo nimalizie yale maboma na nyumba za Walimu. Kuna mahali Kiteto ukipeleka Mwalimu anang’ang’ania suruali ya Mkurugenzi na gari aliyoshuka nayo ni porini, hakubali kukaa na hana nyumba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nyumba moja walimu saba, maboma yameshindikana kukamilika, hatuna nyumba za Walimu, wananchi wamechanga wamefikisha mahali haiwezekani, nipeni special funds. Rural areas kama ya Kiteto ni special na watumishi wengi hawakubali kwenda wanaogopa, wengi wameolewa, wameondoka. Sasa tupeni watumishi na tujengeeni yale maboma ya nyumba za Walimu, Walimu wakubali kukaa, inafika mahali wanaogopa, ikifika jioni anaogopa, shule nyingi zipo porini, sasa zile shule zilizopo porini…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)