Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuchangia Wizara ya TAMISEMI na Utumishi wa Umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hizi ni nyeti sana kwa sababu ni Wizara ambazo zinaleta maendeleo ndani ya nchi yetu. Kwanza kabisa nitoe pongezi kubwa kwa Mheshimiwa Rais wetu John Pombe Magufuli kwa kazi yake nzuri anayoifanya. Pia nitoe pongezi kwa Mawaziri wote kwa ujumla wake, sana kwa Mawaziri hawa wa Wizara ambazo tunazijadili leo hii. Mheshimiwa Waziri Jafo kwa kweli kazi unafanya vizuri na Naibu Mawaziri wote wawili kazi wanafanya vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Wakuu wa Mikoa nawapa pongezi sana kwa sababu nikitoa mfano, Mkuu wangu wa Mkoa wa Iringa, Mheshimiwa Amina Masenza anafanya kazi nzuri sana nampa pongezi. Vilevile DC wetu pamoja na Mkurugenzi wetu, wote wanafanya kazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema utawala bora lazima tuwe makini sana. Kwanza wewe unayejadili utawala bora lazima ujipime. Kwa mfano, hawa watu niliowataja ukiangalia profile yao imesimama iko vizuri na wanafanya kazi nzuri sana. Kwa hiyo, kwenye utawala bora binafsi naona wamekaa vizuri na nchi hii inapiga hatua na tukisema uchumi unakua ni kwa sababu ya utawala bora, kama utawala bora haupo uchumi hauwezi kukua, lakini sasa hivi Tanzania uchumi unakua na sasa tunakwenda 6.8, tuko mbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na haya niliyochangia kwenye utawala bora, naishukuru Serikali kwa upande wa afya kwa kweli wameenda vizuri sana. Nikichukua kwa ujumla wake katika Wilaya yangu ya Mufindi tunaenda vizuri. Serikali imeangalia sana vituo vya afya na wameangalia Tanzania nzima, lakini wamekuja mpaka Wilaya ya Mufindi. Kwenye Jimbo langu la Mufindi wameleta milioni 400 na mpaka sasa hivi kituo cha afya cha Malangali kinatengenezwa vizuri sana na wananchi wanaipongeza sana Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili tunajenga hospitali ya Wilaya ya Mufindi ambayo sasa hivi Serikali imeshatutengea 1.5 billion kwa ajili ya kujenga hospitali ya Wilaya. Tunawapa pongezi kubwa sana, naiomba Serikali tukimaliza ile hospitali ya Halmashauri, naomba ile hospitali ya Wilaya ambayo iko Mafinga basi tuifanye Hospitali ya Rufaa. Tukifanya hivi wananchi wanaweza wakatibiwa vizuri, tukiwa na hospitali ya rufaa tunajua huduma zitakuja zitakuwa nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona kwenye mpango, kwamba mna mpango wa kuboresha vituo vya afya vyote Tanzania nzima vikiwepo na vile vya Mafinga vya Wilaya Mfindi. Jana wakati nauliza swali la msingi niliuliza Vituo vya Afya vya Mninga na Mtwango pale. Bahati nzuri Serikali imejibu vizuri imesema tayari vifaa wameshaandaa na wamesema kufikia mwezi wa Tano watakuwa wameshamaliza, hiyo ni juhudi nzuri sana ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vizuri vinavyofanyika lazima tupongeze ukidharau na kile kizuri wewe tayari unafanya dhambi, binafsi naipongeza sana Serikali na Waziri wa TAMISEMI Mheshimiwa Selemani Jafo, nakuomba sana hivi vituo vya afya ambavyo tayari na fedha unayo na mipango imekaa vizuri, basi umalizie kama ulivyosema mwezi wa Tano utakuwa umemaliza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niongelee kidogo kwenye suala la viwanda, bahati nzuri Wilaya ya Mufindi tuna viwanda vingi sana, lakini tuna kero moja ya ukusanyaji wa kodi TRA pale. Mfanyabiashara anatakiwa alipe kodi lakini asidharaulike, hivyo, wakusanyaji wanaokusanya kodi wasiwadharau wafanyabiashara. Kuna kitu kinaitwa lugha ni kitu kidogo sana, ukienda kukusanya kodi ukisema kwamba asipolipa kodi labda utamfungia biashara yake tayari unamkatisha tamaa. Naiomba Serikali watu wanaotoa lugha mbaya kwa wafanyabiashara wasifanye hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine tunajua tuna viwanda vingi, bahati nzuri naipongeza Serikali na Mheshimiwa alikuwa anasema kule Mkuranga kuna viwanda karibu 80 na Mufindi tuna viwanda vingi tena ni viwanda vikubwa, tukitaja viwanda kuna viwanda vingine ni vikubwa. Kuna kiwanda kimoja mimi sijakipenda sana, kuna hiki kiwanda kinachochinja wanyama wanachinja sana punda, hiki kiwanda sijakipenda. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wanyama ambao wanatumika kwa binadamu kwa kazi za binadamu za kila siku, punda anatumika kubeba mizigo, punda anatumika katika kulima, lakini kwa nini tena punda uanze kumla? Hiyo sijaipenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka miaka ya nyuma Wahehe walikuwa wanachinja mbwa, lakini baada ya kugundua kwamba mbwa ni askari wa kulinda usiku wakaacha kumchinja. (Makofi/Kicheko).

Mheshimiwa Mwenyekiti, utamaduni wetu hatujazoea kuchinja punda, naomba punda wasichinjwe waachwe, kile kiwanda cha punda tusifuate Wachina, kama kwao wanachinja basi wawe ni Wachina, lakini kwetu huku tuna viwanda vingi ambavyo vinaweza vikatuingizia hela nyingi, tuachane na viwanda vya punda hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la maji, Waziri wa Maji nakupongeza sana alikuja kule Mufindi alifanya kazi moja nzuri sana. Ile kazi kwanza Wabunge na Madiwani alitupatia semina Waziri wa Maji ilikuwa nzuri sana. Bahati nzuri tukagawanya fedha tukasema kwamba ile Kata ya Nyororo sasa ipate maji ya gravity kwa sababu tulikuwa tunachimba tu visima na akasema tuachane na visima sasa maji ya bomba yatakuwepo, mlolongo ulikuwa mzuri sana pale Igowole tukafanya vilevile na mradi wa Sawala tukafanya vilevile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri wa Maji sasa kwa sababu fedha zipo, naomba usimamizi uende speed kwa vile tulisema kufikia mwezi wa Sita na Saba ile miradi itakuwa imekamilika. Sawala Mkandarasi yuko site, lakini bado speed ile ndogo sana, kwa sababu manunuzi tu yanachukua karibu miezi miwili. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI kwa sababu system ya maji na vituo vya afya viko kwako tunaomba usimamizi wa maji ukae vizuri kama tulivyokuwa tumeahidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna masuala ya barabara hasa zile za vijijini. Barabara tumepeleka TARURA lakini usimamizi bado unalega sana kwa sababu zamani kwenye Halmashauri tulikuwa na mpango kila mwaka barabara zinatengenezwa, unaweza ukaona labda tumepanga barabara tano, kwa mfano pale Mafinga Wilaya ya Mufindi tuna Majimbo matatu kwa kila Jimbo kila mwaka kwa mfano kwa Mheshimiwa Mgimwa zilikuwa zinawezekana kutengenezwa hata barabara tano, kwenye Jimbo langu la Kusini zikatengenezwa barabara hata tano, lakini sasa hivi kwa mfano kwangu inatengenezwa barabara moja tu.

Naomba sasa kuna barabara ya Maguvani inakuja Mtambula mpaka Kilolo, imeharibika haipitiki kabisa na iko TARURA naomba ile barabara itengenezwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna inatoka hapa Sawala inaenda Kata ya Luhunga mpaka kule Iyegelo, ni mbovu na maeneo yale kuna wakulima wa chai, wanashindwa kusafirisha chai, naomba ile barabara itengenezwe. Inaanzia Sawala inaenda kata ya Luhunga mpaka Iyegelo kuna wakulima wamekamilika, ni wafanyabiashara wazuri sana, sasa naomba TAMISEMI isimamie ile barabara iweze kutengenezwa vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine tuna ujenzi hospitali kubwa, bahati nzuri Serikali niipongeze mlishatutengea 1.5 bilioni, tunategemea mwaka huu tunaanza kujenga ile hospitali na niliomba ramani, mkitupatia mapema sana nategemea haiwezi kuchukua mwezi mzima kutafuta ramani tu, hiyo just a week labda wiki mbili, tatu ili tuanze ujenzi, wananchi kule wamelipokea vizuri sana, Wilaya ya Mufindi nzima wamewashangilia, wakati Waziri anajibu swali waliwashangilia sana wananchi kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wameshaleta proposal tayari kwa Wabunge, wamesema ile hospitali ikijengwa basi hospitali ya Mafinga itakuwa Hospitali ya Rufaa na Mheshimiwa Mgimwa Mbunge wa Jimbo la Kaskazini tulikuwa tumekaa tumejadili kwamba ile hospitali tukikamilisha itasaidia Wilaya nzima na hospitali ya Mafinga tutawapunguzia idadi ya wagonjwa kutibiwa pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Chumi kila siku analalamika hapa anasema ile hospitali inazidiwa, lakini kama hospitali ya Mafinga kwa mfano wagonjwa wale wakatibiwa kwenye hospitali hii ambayo tunajenga na hospitali ya Mafinga ikawa Hospitali ya Rufaa na ikaongezewa huduma tukapata Madaktari, basi Majimbo haya yatakuwa yamekaa vizuri na Wilaya nzima itakuwa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, Serikali imepanga vizuri sana kwamba watatuletea fedha, lakini fedha zije haraka, bahati nzuri wananchi wa Wilaya yetu ni waaminifu sana walitoa eneo bure bila compensation, walitoa bure wakasema kwa sababu tunajenga hospitali, basi ngoja tutoe eneo, tumepewa tayari kubwa. Kwa hiyo, naipongeza Serikali kwenye hilo kwamba itasimamia vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho niongelee suala la umeme. Kwanza Serikali imefanya vizuri sana, watu wa REA wako speed na bahati nzuri wamezunguka katika Majimbo yote. Jimbo la Kaskazini wameenda kwa Mheshimiwa Mgimwa, kwangu Kusini kule wamekuja, katika vijiji vyote wanafanya vizuri, lakini kuna changamoto moja imejitokeza; wale wataalam wakifika pale kufanya survey walikuwa wanaishia sehemu; wanaonesha kwenye vitongoji vingine walikuwa hawendi, kwa hiyo kuna vitongoji bado havijafanyiwa survey. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Wabunge tutaandika vitongoji vyote ambavyo hawajafanya survey ili tukuletee Waziri wa Nishati aingize kwenye ule mpango wa REA ili viweze kupewa, bahati nzuri Waziri wa Nishati yuko vizuri, hotuba zake huwa nazifuatilia vizuri sana na anafanya ziara kila Jimbo hata kwangu alishakuja pamoja na Naibu wake, wote wawili wako vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia speech zao ukizisikiliza ziko vizuri, walisema kwamba siyo issue ya kuweka nguzo watu tukaangalie nyaya walisema ni issue ya kupeleka kwenye kaya, tuone nyumba by nyumba zina umeme na wananchi nimeshawaambia nitapita kila nyumba nione kuna umeme unawaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga hoja kwa mikono miwili. Ahsante sana.