Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. SABREENA H. SUNGURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa, napenda kumpongeza Rais mpya wa Tanganyika Law Society kwa ushindi huo mnono. Tuko pamoja naye sisi kama timu ya wanasheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa masikitiko yangu makubwa na kumpa pole Kamanda wetu na Waziri Kivuli wetu na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni Mheshimiwa Tundu Lissu kwa madhila yaliyomkuta hapa Dodoma. Suala hili limeshakuwa komavu, ni suala ambalo katika jamii yetu ya Watanzania limekomaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kugusia Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Article 14 inazungumzia right to life. Kila Mtanzania ana haki ya kuishi na wajibu wa kutoa roho ni kazi ambayo inafanywa na Mwenyezi Mungu, lakini pale inapotokea mtu ameuawa, basi hata kwenye Islamic Sharia, mimi ni msomi wa Islamic Sharia, tunasema kuna option tatu; moja kisasi; mbili kusamehe; tatu, yule aliyemuua mwenzake abebe gharama za kuhudumia familia ya yule mtu aliyoiacha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa suala la kutoa nafsi za Watanzania katika nchi yetu limekuwa ni common. Napenda niipongeze Serikali, mnajua kwamba kila mtu ana haki ya kuishi na ndiyo maana toka kipindi cha Mzee Mkapa, Mzee Kikwete na kuendelea, Serikali haijajaribu hata siku moja kuchukua jukumu la kunyonga, kwa sababu inajua kila mtu ana haki ya kuishi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hii tabia inayoendelea ya watu kunyongwa, watu kutupwa kwenye viroba, kupigwa risasi hadharani, inatutisha sana. Ni tabia ambayo sisi kama Taifa bila kuangalia vyama, sura na rangi lazima tuikemee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, natokea Mkoa wa Kigoma. Mkoa wa Kigoma uko pembezoni mwa nchi, lakini pia tuko karibu na nchi ambazo zimeingia kwenye vita. Tukiangalia sababu ambazo zilifanya watu wetu wengi wapigane huko nchi jirani ni mauaji ya kimya kimya ya watu wasiojulikana. (Makofi)

Kwa hiyo, kama nchini watu wataendelea kufa, kuumia, tusipochukua hatua, sisi tunakaa jirani kule, walikuwa wanakuja wakimbizi, tunawauliza sababu ya vita ni nini? Wanatuambia, tulikaa usiku baba akavamiwa akauawa. Watoto wakiamka asubuhi wanajua ni nyumba fulani ndiyo iliyovamia; kinachofuatia ni kisasi; vikaanza vita vya wao kwa wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba kama Taifa, tuungane, tuhakikishe kwamba tunazuia aina yoyote ya Mtanzania asiweze kuuawa bila sababu. Mambo haya yamekomaa. Juzi juzi tulisikia Mtwara kule mtu kapigwa risasi kwenye kichogo, juzi juzi tumesikia Mwandishi wa Habari katekwa, kaumizwa; Ndugu yetu Alphonce Mawazo, Mwenyekiti wa Geita alipigwa kule hadharani akafariki; Ben Saanane kapotea mpaka leo haonekani. Mambo haya tukiyakalia kimya kama Taifa kwa kweli naamini tutaangamia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini Serikali ina moyo wa dhati ndiyo maana ikafuta adhabu ya kifo. Basi iendelee kusimamia haya mauaji ambayo yanafanywa na kuendelea kuchafua nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nawakumbuka makamanda wetu waliopoteza maisha kule Kibiti. Ni dhahiri sasa, lazima Serikali isimame na Watanzania tusisikie tena vifo vinavyotokea bila sababu ya msingi ili kutii Katiba yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nijielekeze katika Sheria yetu ya Ardhi, katika kifungu cha 167 kinachozungumzia uanzishaji wa Mabaraza ya Ardhi. Kaka yangu Mheshimiwa Cosato pale ameelezea vizuri sana kwamba Mabaraza haya yana upungufu, wengine wakapendekeza yaletwe yafutwe, wengine wakapendekeza hivi na hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mabaraza haya yameanzishwa kwa mujibu wa sheria. Ukiangalia kifungu cha 167(1) tunaona kabisa kwamba vyombo ambavyo vimepewa mamlaka ya kusimamia migogoro ya ardhi inaanza Court of Appeal inakuja High Court of Tanzania, inakuja District, Land and Housing Tribunal, inakuja Ward Tribunal na inakuja Village Land Council.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kusikitika kwa kile kilichotokea kwa mwenzetu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Paul Makonda, miezi miwili iliyopita kuamua kufuta Mabaraza ya Ardhi kinyume kabisa na sheria za nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, chombo pekee chenye mamlaka ya kutunga sheria, chombo pekee chenye mamlaka ya kufuta sheria na chombo pekee chenye mamlaka ya kufanya amendment za sheria ni Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tunaomba Waziri wa Katiba na Sheria atueleze Mkuu wa Mkoa huyu mamlaka ya kufuta sheria za nchi hii anayatoa wapi? Mnataka nani aseme ili basi kila mtu…

T A A R I F A . . .

MHE. SABREENA H. SUNGURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge hili limewahi kumwita Paul Makonda na kumwonya juu ya uvunjaji wa taratibu na sheria za nchi hii na aliomba msamaha akasema kwamba itakuwa ni mwanzo na mwisho, lakini mara baada ya hapo, tunaona Mabaraza ya Kata ya Mkoa mzima wa Dar es Salaam sasa hivi yamesitishwa na hakuna shughuli zinazoendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba ufafanuzi kutoka kwa Mheshimiwa Waziri kwamba ni mamlaka gani yanayompa Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa huyu mamlaka…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)