Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Godbless Jonathan Lema

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arusha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Nina mambo ya msingi sana ambayo nataka niliambie Bunge. Taifa lolote duniani linaweza likaendelea kama utawala wa sheria na Katiba utazingatiwa. Kwa bahati mbaya, mambo ya kisheria na kikatiba yanayokosewa sasa watu wanafikiri ni temporary na wengine miongoni mwenu mnasema ngoja haya mambo yapite awamu hii tu, lakini baadae tutakuja kurudi kwenye line nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wasiwasi wangu ni kwamba kinachoendelea sasa ni tabia ambayo inaanza, wa-Spanish wanasema tabia inaanza kama utando wa buibui na mwisho wake unaishia kama lehemu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kujadili masuala ya Katiba na Sheria bila kuwa na utawala unaoheshimu Katiba, bila kuwa na Bunge ambalo linaweza likasimamia Serikali Kikatiba na Kisheria, Taifa hili litaendelea kwenda mahali pabaya sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi, Mheshimiwa Polepole ametoa maelekezo kwenye vyombo vya habari kwamba Mheshimiwa Mbunge Zitto Kabwe akamatwe na polisi kwa sababu ya kuchambua hoja za CAG. Maana yake nini? Maana yake ni kwamba sasa Polepole hana maana amemwongelea Mheshimiwa Zitto, maana yake anaongelea Bunge hili lisiendelee na uchambuzi wa jambo lolote ambalo ni kinyume na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ilianza humu ndani, maoni yetu ya Kambi Rasmi ya Upinzani mnayafanyia screening, tumeacha kusoma. Sasa imefika mahali Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi anaonya na kutoa maelekezo kwa Jeshi la Polisi limkamate Mbunge anayechambua ripoti ya CAG. Kama kuna wa kwanza kukamatwa, ni aliyepoteza shilingi trilioni 1.5. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongee, nina masuala muhimu sasa kuhusu matumizi mabaya ya sheria hasa Mahakamani na mara nyingi tukiongelea habari ya Mahakama, watu huwa wanakuja hapa wanasema mambo yaliyoko Mahakamani tusiyaongee. Kwa sababu Bunge ndiyo linatunga sheria na Mahakama inakwenda kutafsiri sheria, mambo yaliyoko Mahakamani yasiongelewe kwa kina gani, lazima tafsiri yake ipatikane, lakini uzembe na matumizi mabaya ya sheria Mahakamani, lazima tuyaongee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kuna kesi ya money laundering. Hizi kesi zinatumika kuonea na kutesa wafanyabiashara. Juzi TLS walipitisha azimio Arusha kwa ajili ya kumtetea Wakili Median Mwale. Mwale ana mwaka wa nane Magereza; DPP amesha-enter nolle zaidi ya mara tano. Nolle nyingine imekuwa entered mwaka huu. Huyu mtu mafaili yake yamekwenda mpaka Court of Appeal, vielelezo vimetupwa na Court of Appeal.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni Jaji amemwachia na Ofisi ya DPP ikasema ukimwachia huyu mtu, hatutamkamata tena. Kwa miaka nane Ofisi ya DPP imeshindwa ku-establish evidence ya kumfunga mtu, bado yuko ndani kama mahabusu. Siyo yeye tu, ilipotokea ya Mwale, watu walifikiri ni Mwale peke yake. Leo kuna Dkt. Ringo Tenga, kuna Sioi, kuna akina Kitillya; hawa ni wale ambao magazeti yanawaandika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimekwenda Magereza nimekuta watu wana money laundering ya shilingi 800,000 M-pesa. Nimemkuta mtu yuko Magereza kwa money laundering ya dola 1,500. Ukishapelekwa kwenye Mahakama ya chini, wanasema hatuna mamlaka ya kusikiliza shauri hili. Mtu anakaa jela miaka nane. Suala hili nimeshaongea na Mheshimiwa Waziri mara nyingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natetea kwa sababu moja, najua mateso ya Magereza. Leo tuna kesi ya Mheshimiwa Mbowe, hii kesi kwenye penal code ikiwa watakutwa na hatia, watakwenda jela mwaka mzima. Hakimu anatoa masharti ya Waheshimiwa Wabunge kuripoti Kituo cha Polisi kila Ijumaa. Haya ni matumizi mabaya ya sheria, matumizi mabaya ya Hakimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiongea hivyo ninyi mnasema hivi, kama hamkuridhika na masharti haya, nendeni kwenye Appellate Court. Kama remedy yetu itakuwa ni kwenda Appellate Court, lakini bila kuwakemea Mahakimu wanao-abuse sheria, wanao-abuse power, maana yake watu wataanza kuiona Mahakama haitendi haki. Mahakama ikipoteza trust, nchi hii itaingia kwenye civil war.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo una Wabunge ambao wana kesi ya mkusanyiko usio halali. Wakikutwa na hatia ni mwaka mmoja jela, unawapa masharti ya dhamana kila Ijumaa Waheshimiwa Wabunge waende Kituo cha Polisi Dar es Salaam. Leo Mheshimiwa Heche ni Mbunge wa Tarime, maana yake kuanzia Jumatano ya kila wiki, kesi ikichukua miaka miwili Jumatano ya kila wiki anaanza safari kutoka Tarime kuja Dar es Salaam. Mambo haya yanaleta maumivu makali sana kwetu sisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nasema hivi, pamoja na kwamba ni kweli Mahakama ni mhimili mwingine, lazima kuwepo na check and balance. Hakimu alinipeleka Magereza mimi kwenye kesi ambayo nilikuwa nimeingia nasikiliza, anamwambia State Attorney usini- mislead kama mlivyoni-mislead kwenye kesi ya Lema. Nimekaa jela miezi minne kwa sababu ya makosa ya Hakimu. Mahakama ya Rufaa inakuja kuamua ndiyo, lakini mtu ameshaumia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Sugu, ameomba, huyu kesi yake akikutwa na hatia amefungwa miezi mitano. Alinyimwa dhamana kwenye kesi ambayo akikutwa na hatia anafungwa miezi mitano, Hakimu anasema huyu akae ndani kwa usalama wake. Huyu anamaliza kifungo kesho kutwa, rufaa yake haijasikilizwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema Serikali inaingilia Mahakama, ni mikakati kama hii tunayoiona kwamba Mheshimiwa Sugu sasa rufaa yake ikisikilizwa mwezi unaokuja na anatoka tarehe 20, atakuwa amepata remedy gani katika kifungo ambacho alikuwa ametumikia?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge, mambo haya siyo ya CHADEMA, ni yetu wote. Utakapokuwa na Mahakama huru, Ofisi ya DPP huru, Ofisi ya AG huru haiwasaidii CHADEMA. Mimi naweza nikaamua leo nikaja huko CCM, lakini haijalishi. Unapokuwa na Mahakama ambayo haiko huru, unakuwa na mazingira mabaya ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Polisi hawako huru; juzi mmemwona Makonda na sinema yake ya watoto. Leo wamemkamata yule dada waliyekuwa wamempa deal aseme ni mtoto wa Mheshimiwa Lowassa, anakamatwa tena kwa sababu alikanusha juzi. Haya matumizi mabaya ya sheria ambayo sasa yanaingia Mahakamani. Watu wanaozea jela. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, money laundering, Waheshimiwa Wabunge msipolileta humu Bungeni, Bunge liweze kuichambua na kutolea maelekezo mapya, hii kesi haitamwacha Mbunge yeyote salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana nimeona barua ya TRA; mtu kanunua nyumba ya shilingi milioni 80 Sinza. TRA wanaandika barua, wanakwambia badala ya ku-claim capital gain, wanaenda kuandika barua wanasema, tunataka uje utuambie na chanzo cha fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi siku nikifanya hivyo, mkatafuta chanzo cha fedha, Mheshimiwa Jenista Mhagama mimi nitasema umenihonga wewe ama Mheshimiwa Angellah Kairuki, sasa sijui hiyo kesi itaendeshwaje? (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo siyo tu yanaua uchumi, haya mambo yanaondoa confidence kwa wafanyabiashara. Mimi nawaambia, leo watu nchi hii wanahamisha fedha kwa sababu ya sheria za ajabu ajabu. Hakuna tena transaction zinazopita kwenye mabenki. Ukiweka shilingi milioni 20 kwenye akaunti; mimi nili-transfer hela kwenye akaunti yangu wanazuia, tueleze sababu ya ku- transfer hela. Napeleka hela kwa mke wangu unaniuliza sababu? Sababu inaweza ikawa love. Haya mambo yanafanya watu sasa wasiweke hela benki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, TAKUKURU, hizi tax holdings zilizoundwa ambazo ziko chini ya Kamati ya Ulinzi wa Mkoa huko zinafanya watu wanakuwa na hofu. Transaction hazipiti kwenye mabenki, benki wanakosa deposits, benki sasa zinaanza ku-fail.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuomba sana, Mheshimiwa Waziri, punguza uoga.