Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Mungano na Mazingira kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Mungano na Mazingira kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nami naomba nichangie kwenye jambo hilohilo la kuzalisha umeme kwenye Mto Rufiji na nitachangia zaidi katika muktadha wa uhifadhi na ikizingatiwa kwamba mradi huu unatekelezwa kwenye eneo la Hifadhi ya Pori la Akiba la Selous ambalo lipo chini ya Usimamizi wa Wizara yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na umuhimu na uthamani wa kipekee ambao unawekwa kwenye Pori la Akiba la Selous, lakini naomba Bunge lako Tukufu na Watanzania wote kwa ujumla watambue kwamba Selous ni rasilimali ya Taifa na rasilimali zina sifa moja ili ziwe rasilimali; zinapaswa kuleta manufaa kwa wananchi, zinapaswa kuleta manufaa kwa binadamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba tutambue kwamba rasilimali ambazo tumejaliwa kama urithi katika nchi yetu haziwezi kututenganisha na mahitaji ambayo sisi tunahitaji kuyapata kutokana na rasilimali ambazo tumepewa kama zawadi. Kwa hiyo, ni lazima tuwianishe uwepo wa rasilimali na maendeleo ya watu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna schools of thought mbalimbali, kuna watu wanaoamini kwamba rasilimali zihifadhiwe kama zilivyo mpaka mwisho wa dunia, lakini wanasahau kwamba na sisi binadamu ni sehemu ya dunia, ni sehemu ya ikolojia na tuna mahitaji yetu na kwa maana hiyo ni lazima na sisi tutumie rasilimali hizi. Kitu cha msingi cha kuzingatia ni kuhakikisha kwamba tunatumia rasilimali kwa uendelevu wake bila kuziharibu, bila kuathiri bionuwai nyingine iliyopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilihakikishie Bunge lako Tukufu hapa kwamba Serikali kupitia Wizara yetu imezingatia matakwa ya uhifadhi endelevu wa rasilimali iliyopo kwenye Hifadhi ya Taifa ya Pori la Akiba la Selous. Tumefanya hivyo kwanza kwa kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa kufuata misingi ya utekelezaji wa miradi. Ndiyo hiyo Environmental and Social Impact Assessment anayoizungumzia Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati. Hilo ni hitaji la kwanza la lazima na tumesema itafanyika kwa haraka na ikamilike kabla utekelezaji wa mradi haujaanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la pili, Waziri wa Maliasili na Utalii nimeunda kikosi kazi cha Wataalam kutoka Taasisi za TAFIRI TAWIRI, TITISA na Taasisi nyingine zinazohusika na maliasili ili wafanye utafiti wa kina wa kuangalia bionuwai iliyopo katika eneo husika. Utafiti huu utatuwezesha kujua kuna species gani zipo katika eneo la utekelezaji wa mradi na tufanye nini tuweze kuzihifadhi zisipotee na nini kitatokea kama tutafanya mradi huu kwa zile species zilizopo pale. Je, species zilizoko pale ni endemic kwa maana pale ni makazi yao ya kudumu ama ni species hizi ambazo exotic ambazo zimekuja kuhamia kwa kufuata mahitaji mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiweza kuzitambua hizo species na mahitaji yake na kujua kama endemic ama ni exotic tutaweza kujua tufanye nini ili kuokoa zisipotee na ndiyo kazi ambayo sisi Wizara yetu tunafanya kuhifadhi bionuwai mbalimbali za wanyama pamoja na mimea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo kuna timu ya Wataalam iko site, inakusanya mbegu za wanyama, samaki na mimea na kila aina ya bioanuwai iliyoko pale na kuzitunza kwa ajili ya matumizi ya baadaye. Pia tumehakikisha kwenye design ya mradi kutabaki na Oxbow Lakes, maziwa ya asili yaliyoko pale, lakini pia tunaongeza maziwa mengine ambayo yatasaidia kuweka uhai wa viumbe hai ambavyo viko katika eneo lile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba niwatoe hofu Waheshimiwa Wabunge kwamba Serikali iko macho na sisi wahifadhi tuko macho hatutokubali Pori la Akiba la Selou lishuke hadhi yake kwa sababu ya utekelezaji wa mradi huu. Madhara yanaweza yakajitokeza, lakini mpaka sasa hakuna anayejua ni nini kitatoke kwa sababu hakijatokea. Kwa hivyo, nyingi zinazozungumzwa hapa kwa mfano mchango wa Dkt. Sware ni nadharia tu, ni theory’s tu ni rhetoric hakuna ushahidi wa nini kitatokea kwa hakijatokea na uharibifu haujafanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo tunachokifanya kwa sasa ni kujipanga kupunguza madhara yanayoweza kutokea endapo mradi utatekelezwa ndicho tunachojipanga. Kuna nadharia kwamba joto litaongezeka kwa sababu ya utekelezaji wa mradi, kuna nadharia kwamba flow ya mto itabadilka kutokana na utekelezaji wa mradi. Zote ni nadharia, huwezi kuwa na uhakika kwamba zitaathiri mto pamoja na wanyamapori kwa namna gani, sambamba na hilo. (Makofi)

T A A R I F A . . .

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa yake siipokei na sipokei kwa sababu za kisayansi kama yeye ni Dkt na mimi ni Dkt. vilevile na mimi ni mwanasayansi, nampa sababu ya kisayansi kama yeye ni daktari anaamini kwenye sayansi,, tusikilizane kama yeye ni daktari na anaamini kwenye sayansi nampa sababu ya kisayansi, hakuna haja ya kubishana kwa kelele, tulieni msikie sayansi. Anachokisema kinaweza kikatokea ndiyo ninachosema kwamba ni nadharia, ni theory hakijatokea bado kwa sababu mradi haujatekelezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namalizia kuna kitu kitakachojitokeza ni kwamba wanyama, mimea wana kitu kinaitwa adaptation, kwenye mabadiliko yanayojitokeza. Kwa hivyo mazingira yatakapobadilika wale wanyama wanabadilisha tabia zao wanaweza waka-adapt kwenye mazingira mapya yaliyojitokeza. Kwa hiyo,hiyo ni sababu ya kisayansi na nina uhakika anaifahamu. Kwa hivyo hatuna haja ya kubishana sana kwa sababu hii ni sayansi.